Nafasi Ya Matangazo

October 26, 2017


Fainesy Matiholo mshindi wa 12 wa droo kubwa ya Tatu Mzuka na kujinyakulia kitita cha shilingi za Kitanzania Milioni 65.

Mheshimiwa Queen Mlozi Mkuu wa Wilaya wa Tabora akitoa zawadi kwa Fainesy Matiholo akimuakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mheshimiwa Aggrey Mwanri.Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ofisi za Mkoa wa Tabora.

Fainesy Matiholo akishangilia ushindi wake wa kitita cha Milioni 65 akiwa baba na Mama yake Tabora Mjini.
*****************
Fainesy Matiholo, mkazi wa Tabora Mjini ambaye amekuwa akicheza Ttau Mzuka huku akiwaa kuwa itatokea siku aibuke msndini basi, siku hiyo ikawa ni Jumapili iliyopita ambapo akaibuka kuwa mshindi wa 12 wa droo kubwa ya Tatu Mzuka na kujinyakulia kitita cha shilingi za Kitanzania Milioni 65.

Bi. Matiholo amekabidhiwa zawadi yake ya ushindi na Mkuu wa Wilaya ya Tabora Mheshimiwa Queen Mlozi ambaye alitoa zawadi hiyo akimuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mheshimiwa Aggrey Mwanri. Makabidhiano hayo yalifanyika katika Ofisi za Mkoa wa Tabora.

“Nimekuwa nikicheza Tatu Mzuka kila juma lakini lengo langu kubwa lilikuwa kupata ushindi wa kila saa. Sikutarajia kabisa kuwa nitaibuka mshindi wa droo kubwa ya Tatu Mzuka,” anasema.

Katika hafla hiyo ya kukabidhi zawadi, mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bi. Mlozi alizungumza kuwa; “tumefurahi sana kuona kuwa juma hili mshindi wa Tatu Mzuka katika katika Mkoa wetu. Ushindi huu umetusaidia kuamini kuwa mchezo huu unatoa fursa sawa kwa watu wote. Naamini sasa wananchi wa Tabora watahamasika zaidi kushiriki katika mchezo huu.”

Katika ushindi huu wa Bi. Matiholo pia rafiki zake watatu ambao hushiriki kucheza Tatu Mzuka nao wamefanikiwa kujishindia kiasi cha Shilingi milioni 1 kila mmoja kupitia kipengele cha Tatu Mzuka “cheza na washkaji na washikaji promosheni.” Walioshinda kipengele hiki ni Jacqueline Samuel, Sande Kabaye na Lilian Tegete.

“Tatu Mzuka imebadili maisha yangu,” Bi. Matiholo anasema na kuongeza kuwa; “naweza sasa kuanza kupanga namna ya kuishi maisha bora zaidi, nitaweza kumpatia mwanangu elimu bora zaidi na pia kuboresha biashara yangu,“ alieleza.

Hata wewe unaweza kuwa mshindi ajaye wa Tatu Mzuka na safari hii mshindi anatarajiwa kupata kitita kinachofikia milioni 110. Hadi sasa kumekuwepo na washindi zaidi ya milioni 1.7 waliojishindia zawadi mbalimbali kutoka Tatu Mzuka. Pia kuna zaidi ya shilingi milioni 500 zinazosubiriwa kushindaniwa kadri siku zinavyoenda. Unaweza kuwa mshindi lakini jambno la kufanya ni kushiriki mchezo huu mara nyingi zaidi uwezavyo.
Posted by MROKI On Thursday, October 26, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo