Kama ilivyo
ada, King’amuzi cha DStv kitaonyesha mubashara mechi inayosubiriwa kwa
hamu kubwa kati ya Tanzania na Zambia ikiwa ni nusu fainali ya michuano
ya COSAFA 2017 itakayochezwa kesho Jumatano
saa 12 jioni huko Afrika Kusini
Taifa stars
imefuzu nusu fainali baada ya shughuli pevu ya kuwafunga wenyeji Africa
Kusini (Bafana Bafana) na sasa itakumbana na moja ya miamba ya soka
barani Afrika Zambia katika nusu fainali inayotarajiwa
kuwa na upinzania mkali.
Meneja
Masoko wa Multichoice Tanzania Alpha Mria amethibitisha kuwa mechi hiyo
itarushwa mubashara kupitia DStv chaneli ya SuperSport4 ambayo
inapatikana kwenye vifurushi vyote kikiwemo kile cha DStv
Bomba ambacho hupatikana kwa Sh 19,975 tu.
“Kwanza
kabisa tunawapongeza sana Taifa Stars, wamefanya kazi kubwa, wameleta
matumaini makubwa, sasa kazi ni moja tu, kwenda fainiali na sisi DStv,
tunawahakikishia wateja wetu na watanzania kwa
ujumla kuwa mtanange huo watauona mubashara kupitia DStv” alisema
Alpha.
Ameongeza
kuwa enzi ya watanzania kusubiri matokeo ya michuano mikubwa kama hii ka
saa kadhaa baada ya mechi kukamilika umepitwa na wakati, kwani kwa
DStv, michuano hiyo huonyeshwa moja kwa moj. “Hakuna
tena kwend amtandaoni kuangalia matokeo, wala kumuuliza mtu, ukiwa na
DStv, unashuhudia mwenyewe” alisema.
Huduma za
DStv zimekuwepo hapa Tanzania kwa miaka 20 sasa na maelfu kwa maelfu ya
watanzania wameunganishiwa huduma za DStv na kuwafanya mamilioni ya
watanzania katika kila pembe ya nchi kufurahia
huduma zake. Mbali na kujikita Zaidi katika michezo na burudani, DStv
pia ina chaneli mbalimbali za habari, Sanaa, Dini, Utafiri, Sayansi na
Teknolojia, na pia utamaduni.
0 comments:
Post a Comment