Nafasi Ya Matangazo

October 23, 2016

 Wahitimu katima Shule ya Sekondari ya Abbey Abasia wakionesha mambo mbalimbali waliyojifunza katika masomo ya Sayansi.
Wahitimu wa kudato cha nne katika Shule ya Sekondari ya Abbey Abasia wakiwa katika maandamano kabla ya kuanza mahafali yao.
 
Mkuu wa shule ya sekondari ya Abbey Abasia ya Ndanda, Faza Augustine Ombay akimwonyesha mbunge wa jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe mradi wa maji taka unaojengwa shuleni hapo.
Mbunge wa jimbo la Ndanda, Cecil Mwambe akipokea sehemu ya zawadi ya madawati 50 aliyopewa na uongozi wa shule ya Sekondari ya wavulana ya Abbey iliyopo Masasi wakati wa mahafali ya saba ya kidato cha Nne.Kulia ni Msaidizi wa Abate Abasia ya Ndanda na paroko wa Parokia ya Ndanda,Faza Silvanus Kessy, akifuatiwa na mkuu wa shule,Faza Augustine Ombay.Aliyesimama kushoto ni Diwani wa kata ya Mwena, Nestory Chilumba.
Wanafunzi wa shule ya sekondari ya Abbey iliyopo Ndanda wilayani Masasi wamewataka wazazi kuwaacha watoto wao kujichagulia masomo wanayotaka ili kutimiza ndoto zao badala ya kuwawekea msukumo katika masomo ya Sayansi pekee na kuyaacha masomo ya biashara na sanaa.

Pia, jamii imetakiwa kutambua jukumu la kuwalea watoto ili kuwa na nidhamu ni la wazazi na walezi badala ya kuwaachia walimu pekee kwa manufaa ya kuwa na Taifa bora.

Hata hivyo wazazi wameaswa kipindi  watoto wao wanapokuwa likizo wasiwapeleke kwenye masomo ya ziada maarufu tuition na badala yake wawapatie kazi za nyumbani kwani wanachanganywa na masomo ya ziada.

Wito huo umetolewa na msaidizi wa Abate Abasia ya Ndanda na paroko wa parokia ya Ndanda,Faza Silvanus Kessy wakati wa mahafali ya saba ya kidato cha nne shuleni hapo na kuwataka wazazi na walezi wote wanaowasomesha watoto wao shuleni hapo kuacha kuwapeleka katika masomo ya ziada.

“Nidhamu ya ndio  matokeo mazuri kama atakuwa na ushirikiano na mshikamano hawezi kufanya vibaya kwasababu kila atakachoambiwa lazima atafuata ,hivyo ni ,ni jukumu la wazazi pia katika kulea watoto , niwaonye sana na kitu kinachoitwa tuition  (masomo ya ziada) kama una mtoto  wako anayesoma hapa ni marufuku kumpeleka tuition na masomo ya ziada ya mitaani  huko wannachakachuliwa motto anashindwa kujua kipi ni kipi,wakirudi likizo wapeni  kazi za kupika, kufua, kuosha vyombo na bustani,"alisema faza Kessy

Kwa upande wake mkuu wa shule,Faza Augustine Ombay aliitaka seerikali kuacha kuingiza siasa katika masomo kwani wanaharibu mfumo na hivyo kuwelka taifa katika hatari .

"Nimpongeze sana rais katika suala la madawati amefaulu,lakini mbunge wa jimbo la Ndanda uko hapa niwaombe sana nyie ndio wenye bunge tunaiomba  serikali isilete siasa katika elimu  mtaangamiza kizazi cha sasa na kijacho,mkiweka siasa  mtaharibu mfumo na hata kwa  Mungu mtahukumiwa na badala yake waangalie ni kwa namna gani wataboresha miundombinu mingine "alisema Ombay

Matokeo ya mwaka jana ilikuwa na wahitimu 111 ambapo wanafunzi 95 walipata ufaulu wa daraja la kwanza, wanafunzi 14 daraja la pili na wawili daraja la tatu.

Hata hivyo, mgeni rasmi ambaye ni mbunge wa jimbo la Ndanda  Cecil Mwambe, aliwataka wazazi kuwaandalia watoto wao  mazingira mazuri ya elimu   ya chini ili waweze kupata nafasi ya kusoma katika shule hiyo na kuondokana na malalamiko.

"Jamani tuachanae na kulalamika kuhusu watoto wetu kupata elimu inayotakiwa, ifahamike maandalizi yanayofanyika shuleni hapa ni mazuri, elimu bora ni mchakato sisi tulio wengi hatujajiandaa ndio sababu zinazopelekea wahitimu wa ukanda huu kuwa wachache,vigezo vya kuingia Abbey sio dini wala ukabila bali ni ufaulu na nidhamu kwahiyo ndugu zangu tubadilike, "alisema Mwambe na kuongeza:

"Tusiwe watu wa kulalamika,tusidanganyane kuna elimu bora ni lazima iwe ya gharama,wazazi waunge mkono kupata elimu bora tupate wataalamu wa baadaye ,"alisema Mwambe

Hatika hatua nyingien mbunge huyo alimwaguza diwani wa kata ya Mwena, Nestory Chilumba kushirikiana kwa kushirikiana ma kamati ya uongozi ya shule kuona ni kwa namna gani watamaliza tatizo la upigaji wa mziki jirani na shule hiyo hali inayopelekea baadhi ya wanafunzi kutoroka.

Hata hivyo uongozi wa shule hiyo ulitoa madawati 50kwa mbunge huyo kama zawadi ambapo atayagawa katika  baadhi ya shule.
Posted by MROKI On Sunday, October 23, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo