Nafasi Ya Matangazo

March 10, 2016

 Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako  akizungumza na wanafunzi wa chuo cha Kikuu cha St Joseph Dar es Salaam leo na kuwataka kurejea darasani huku malalamiko yao yakitafutiwa ufumbuzi.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St Joseph, Dar es Salaam wakimsikiliza Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako leo.
***************
Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako ameingilia kati mgogoro wa wanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. Joseph Dar es Salaam, waliogomea kufanya mitihani na kuwataka warejee madarasani wakati matatizo yao yakishughulikiwa.

Wanafunzi hao walikuwa katika siku ya tatu ya mgomo wao jana ambapo pamoja na mambo mengine walikuwa wakilalamikia mapungufu yaliyopo chuoni hapo ikiwa ni pamoja na maabara za kufanyia mafunzo kwa vitendo, matatizo ya kiutawala, mitaala ya kufundishia pamoja na ada.

Waziri Prof. Ndalichako aliyewasili Chuoni hapo majira ya Saa 3 asubuhi na kuanza kufanya ziara kukagua mazingira ya kufundishia ya chuo hicho kwa kutembelea maabara zote chuoni hapo na kasha kwenda kuzungumza na utawala, Serikali ya wanafunzi na mwisho alihutubia wanafunzi wote.

Aidha ameiagiza Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), chini ya Katibu Mtendaji wa TCU, Profesa Yunus Mgaya kufuatilia na kuchunguza kwa makini madai ya wanafunzi hao juu ya kuwepo kwa wahadhiri wasio na sifa zinazotakiwa.


Aidha aliutaka uongozi wa chuo hicho chini ya Makamu Mkuu wa Chuo wake Dk Gopal Raju Bhakasaju kuhakikisha yote ambayo wameahidi kuyafanya wanayatekeleza mapema bila kuathiri masomo na hasa kama yatafanyika. 
Posted by MROKI On Thursday, March 10, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo