Nafasi Ya Matangazo

January 18, 2016

Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida akisoma hotuba wakati wa halfa ya kusaini mikataba ya msaada kutoka kwa serikali ya Japan, halfa iliyofanyika kwa balozi jijini Dar es Salaam.

Na Rabi Hume, Modewjiblog
Serikali ya Japan kupitia mfuko wake wa misaada wa Grant Assistance for Grassroots Human Security Projects (GGHSP) imesaini mkataba wenye thamani ya Dola 204,300 sawa na Milioni 430 za Kitanzania kwa ajili ya kusaidia miradi mitatu ya kijamii.

Akisoma hotuba katika halfa ya kusaini mikataba hiyo ambapo Waziri Mkuu mstaafu wa Tanzania, Mhe. Edward Lowassa alikuwa mgeni rasmi, balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida alisema serikali ya Japan imetoa msaada huo kwa kutambua changamoto zilizopo katika sehemu ambazo wanatoa msaada huo na wanataraji utaleta mabadiliko. 
Balozi wa Japan nchini, Masaharu Yoshida akikabidhiana mkataba na Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Theresia Mahongo baada ya kusaini mkataba huo wenye thamani ya Dola 86,182 sawa na Milioni 180 za Kitanzania kwa ajili ya ujenzi katika Shule ya Kingolwira.

Alisema licha ya miradi ambayo serikali yake ya Japan imeweka saini kusaidia shughuli mbalimbali za maendeleo, serikali ya nchi hiyo itaendelea kutoa misaada kwa Tanzania kupitia mfuko huo ili kuzidi kupatikana kwa huduma bora kwa watanzania.


“Ninayo furaha kusaini mikataba mipya mitatu ya misaada kutoka serikali ya Japan kupitia mfuko wa Grant Assistance for Grossroots Human Security Projects (GGHSP).

“Serikali ya Japan itaendelea kutoa misaada katika kusaidia upatikanaji wa huduma za msingi kwa Tanzania kupitia mfuko wa misaada na nimatumaini yangu sherehe ya leo itazidi kuimarisha uhusiano mzuri uliopo kati ya Tanzania na Japan,” alisema Yoshida.
 
Balozi wa Japan, Masaharu Yoshida na Askofu Solomon Massangwa kutoka Arusha Lutheran Medical Centre wakikabidhiana mikataba baada ya kusaini mkataba wa msaada kwa ajili ya Kituo cha Afya cha Lutheran Arusha. SOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Aidha Yoshida aliitaja miradi hiyo kuwa ni upanuzi wa Shule ya Msingi ya Kingolwira ambayo mradi utasaidia ujenzi wa madarasa matatu , ofisi ya mwalimu mkuu na jengo la choo ambapo mradi huo utagharimu Dola za Kimarekani 86,182 sawa na Milioni 180 za Kitanzania.



Mradi wa pili ni ujenzi wa uzio katika Shule ya Msingi Muyuni iliyopo Mkoa wa Kusini Unguja ambapo mradi uagharimu Dola za Kimarekani 29,799 sawa na Milioni 62 za Kitanzania na mradi wa tatu kuwa ni ununuzi wa vifaa katika hospitali ya Arusha Lutheran Medical Centre wenye thamani ya Dola za Kimarekani 88,319 sawa na pesa ya Kitanzania Milioni 185.



Akizungumza na Mo Dewji Blog baada ya kusaini mikataba hiyo, mwakilishi wa Arusha Lutheran Medical Centre, Askofu Solomon Massangwa alisema msaada ambao umetolewa na serikali ya Japan utatumika kununua vifaa vya chumba cha wagonjwa mahututi (ICU).


Balozi wa Japan, Masaharu Yoshida akisaini mkataba pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa TCRA, Dkt. Ally Simba ambaye alimwakilisha mwalimu mkuu wa Shule ya Muyuni katika halfa ya kusaini mkataba wenye thamani ya Dola 29,799 sawa na Milioni 62 za Kitanzania kwa ajili ya ujenzi wa uzio katika Shule ya Muyuni iliyopo mkoa wa Kusini Unguja.

Alisema kwa mwaka 2014 kituo hiyo ilikuwa ikipokea hadi wagonjwa 9000 wa nje na imekuwa ikipokea hadi wagonjwa kutoka nje za nje kama Kenya na hivyo ununuzi wa vifaa hivyo vitasaidia kuwahudumia wagonjwa wanaofika katika kituo hicho cha afya wakiwa mahututi.


“Wametupatia msaada wa wa vifaa vya kwenye vyumba cha wagonjwa mahututi (ICU) na tunawashukuru sana kwa msaada huo na tunaamini utasaidia kuokoa maisha ya wananchi wengi wanaofika kituoni kwetu kupata matibabu,” alisema Askofu Massangwa.
 Balozi wa Japan, Masaharu Yoshida akiwa kwenye picha ya pamoja na mgeni rasmi katika halfa hiyo, Waziri Mkuu mstaafu, Mhe. Edward Lowassa wakati kusaini mikataba ya miradi mitatu yenye thamani ya Dola 204,300 sawa Milioni 430 ya Kitanzania kwa ajili kusaidia Shule ya Kingolwira, Shule ya Muyuni na Kituo cha Afya cha Lutheran kilichopo Arusha. 


Nae mwakilishi wa Shule ya Kingolwira, Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro, Theresia Mahongo alisema msaada huo watatumia kama jinsi umevyokusudiwa kwa kujenga majengo mapya lakini pia kutengeneza madawati ili kupunguza tatizo hilo shuleni hapo na kuwataka wadau wa elimu mkoani Morogoro kujitoa kusaidia sekta ya elimu mkoani humo.


Nae Mwalimu Mkuu wa Shule ya Mbuyuni, Saleh Hamad alisema msaada huo umewafikia kwa muda muafaka kipindi ambacho wamekuwa na mahitaji makubwa ya ujenzi wa uzio katika shule hiyo kutokana na mazingira yaliyopo shuleni hapo na hivyo kuishukuru serikali ya Japan kwa msaada imeowapatia na kuahidi kuitumia kama walivyokusudia kutumika.
Posted by MROKI On Monday, January 18, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo