Nafasi Ya Matangazo

September 23, 2015

NIZIARA ya kwanza ya kihistoria kwa kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis kuzuri Marekani tangu achaguliwe kushika wadhifa huo. 


Papa Francis mwenye umri wa miaka 78, ameingia nchini marekani jana baada ya kumaliza ziara yake ya siku nne nchini Cuba ambako atakaa kwa siku tano atakuwa katika miji ya Washington DC, New York na Philadephia ambako pia  maadhimisho ya Umoja wa Mataifa ambapo zaidi ya viongozi wa juu Duniani 100 watakuwa katika mji huo wa New York.

Lakini tofauti na viongozi wengine mbalimbali wanaowasili nchini humo na kupewa heshima kubwa na ya mapokezi huku wakitumia magari ya kifahari, Papa Francis ameweka rekodi na kuwa kiongozi pekee aliyeamua kutumia gari dogo aina ya Fiat 500 rangi nyeusi.

Akiwasili katika uwanja wa Ndege wa kijeshi wa Andrews uliopo mjini Washington, Papa Francis alipokelewa na mwenyeji wake Rais Baraka Obama wa Marekani kisha kumtambulisha kwa mkewe na familia yake, Makamu wa Rais Joe Biden kisha viongozi wengine wa juu wa taifa hilo na kuondoka uwanjani hapo wakiwa katika magari tofauti.

Papa Francis ambaye kwa kawaida ni mnyenyekevu,  aliondoka kwa kutumia gari hilo dogo Fiat 500 huku likisindikizwa na kulindwa vilivyo na magari ya usalama na Rais Baraka Obama akiondoka katika gari lake aina ya Beast ambalo kamwe haliwezi kutetereka na bomu la aina yeyote kwa jinsi lililovyotengenezwa.

 Papa akiondoka akiwa ndani ya kari dogo aina ya Fiat 500
 Alipowasili uwanjani hapo huku akilakiwa na Rais Barack Obama wa Marekani, Familia yake na viongozi wengine wa juu wa Marekani.

 
 Rais Barack Obama akisalimiana na Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis.
 Papa Francis akiwa mwenye furaha na mwenyeji wake
 Akisalimiana na Familia ya Rais Barack Obama.
 Papa akiondoka
 Gari lililo mbeba Papa Francis likiondoka uwanjani hapo.
Msafara wa Papa mitaa ya D.C.
Posted by MROKI On Wednesday, September 23, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo