Nafasi Ya Matangazo

May 01, 2015

Mwandishi wa habari mkongwe Kyaloeichi Oko Kessy (62) amefariki usiku wa kuamkia jana nyumbani kwake Pugu jijini Dar es Salaam.
 
Mpwa wa marehemu Tumaini Msengi alisema leo kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu kwa muda mrefu na amekuwa akitibiwa katika hospitali mbalimbali za jijini Dar es Salaam hadi jana ambapo mauti yalimkuta.
 
Kabla hajaanza kuugua Kessy alikuwa mwandishi wa kujitegemea akiandika zaidi uchambuzi na makala katika vyombo mbalimbali vya habari nchini yakiwemo magazeti ya Motomoto,Shaba,Rai, na mengineyo mengi pia alikuwa ni mtunzi wa vitabu vya aina mbalimbali.
 
Msengi ameeleza kuwa  marehemu ameacha watoto wawili na mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa mdogo wake Chanika nje kidogo ya jiji na mazishi yanatarajiwa kufanyika wiki ijayo.
 
Marehemu ni mzaliwa wa kijiji cha Rosho Kilema mkoani Kilimanjaro.
 
 Bwana alitoa na Bwana ametwaa, Jina la Bwana lihimidiwe.

Mawasiliano zaidi 
Tumaini  Msengi (mpwa wa marehemu)-0713233120
Victor Muhanika-0784426865
Posted by MROKI On Friday, May 01, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo