Nafasi Ya Matangazo

March 31, 2015

 Mbunge wa Nzega, Hamisi Kingwangala akiuliza swali Bungeni mjini Dodoma.

 Wabunge wakitoka Bungeni jana baada ya Bunge kuahirishwa kwa muda.


Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Mchemba akijibu maswali Bungeni yaliyoelekezwa katika wizara hiyo
 Mbunge wa Viti Maalum, Rita Kabati (kulia) akiwa na Mbunge mpya wa kuteuliwa, Dk Grace Puja Bungeni mjini Dodoma
Mbunge wa Ubungo, John Mnyika (kushoto) akitoka Bungeni jana na mbunge mwenzake wa Iringa mjini, Mchungaji Peter Msigwa.

Wabunge wa kutoka kulia, Mbunge wa Muhambwe, Felix Mkosamali, Ezechiel Wenje na Mbunge wa Ngara, Deogratius Ntukamazima wakimpongeza Mbunge mpya wa kuteuliwa, Innocent Sebba baada ya kula kiapo Bungeni mjini Dodoma

Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akiteta jambo na Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Juma Nkamia Bungeni mjini Dodoma
 Wabunge na Mawaziri mbalimbali wakifuatilia mijada ya Bunge, Bungeni mjini Dodoma jana.
Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments
 Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda.

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda (kushoto), akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari ofisini kwake Dar es Salaam jana, wakati akitoa tamko la wilaya hiyo kuhusu uzinduzi wa siku ya upandaji miti itakayofanyika kesho  kimkoa eneo la Mabwepande wilayani humo. Kauli mbiu ya siku hiyo ni 'Panda Miti, Miti ni Hazina 
 *************
WANANCHI wametakiwa kupanda miti na kuitunza ikiwa ni kudumisha matumizi endelevu ya misitu kwa kizazi kilichopo na kijacho.

Mwito huo umetolewa Dar es Salaam jana na Mkuu wa Wilaya ya Kinondono, Paul Makonda ambapo alisema maadhimisho ya siku ya kupanda miti, kauli mbiu mbiu yake ni Panda Miti, Miti ni Hazina.

Makonda alisema lengo ni kuelimisha, kuhamasisha, na kuikumbusha jamii umuhimu wa kupanda miti ambapo kilele cha maadhimisho yatafanyika mkoa Dar es Salaam, wilaya ya kinondoni, katika shule ya msingi Mjimpya kata ya Mabwepnde.

"Kila mmoja wetu anafahamu kuwa miti ina faida nyingi kwa jamii yetu ikiwemo kutupatia matunda, kivuli, dawa za asili, mapambo, kuzuia mmomonyoko wa ardhi, hewa safi, kuni, mkaa na mbao,".

Alisema misitu inahifadhi wanyama pori ambao ni kivutio kwa watalii wanaotupatia fedha za kigeni hivyo kila mmoja anawajibu wa kudhamini uwepo wa miti katika mazingira yake.

Aidha Makonda alisema miti ipandwe kwa mpangilio na kuzingatia ikolojia yake, na kuifanya hamashauri ya ya manispaa ya konondoni inakuwa na madhari nzuri na kuvutia.

Alisisitiza kuwa si vizuri kupanda miti mikubwa katikati ya barabara na karibu na nyaya za umeme, ambazo zinaweza kusababisha madhara hususan katika kipindi cha mvua. (Imeandaliwa na mtandao wa www.habari za jamii.com)
Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments
 Wanafunzi wa Chuo cha Utumishi wa Umma Tabora wakiwa na Mbunge wa Tabora Mjini, Alhaji Ismail Aden Rage walipotembelea Bungeni mjini Dodoma hii leo kwa ziara ya kimafunzo.
Wanafunzi hao walitembelea maeneo mbalimbali ya Bunge pamoja na kujifunza shughuli za Bunge zinavyofanyika.
Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments

IMG_8907
Mama Hadija wa Unga  LTD jijini Arusha akiwa anaangalia zawadi la kapu baadaya kuibuka mshindi kwa kusikiliza Radio 5 kipindi cha taarifa ya habari na matukio,pembeni ni watoto wakiwa wanashuhudia zawadi hizo
IMG_8909
Watangazaji wa kituo cha  Radio 5 wakamkabidhi mshindhi wa pili mama Hadija wa Unga LTD  kapu la zawadi baadaya kuibuka mshindi kwa kusikiliza Radio 5 kipindi cha taarifa ya habari na matukio.
IMG_8926
Kulia ni Hilda Kinabo,kushoto Wilfredy watangazaji mahiri wa kituo cha Radio 5 wakimkabidhi mama Ruthi Sumary mkazi wa Sokon 1 zawadi ya Pasaka
IMG_8928
Watangazaji wa kituo cha Radio 5 wakimkabidhi mshindi wa 3 mama Ruthi Sumary mkazi wa Sokon 1 Kapu la zawadi ya Pasaka baada ya kuibuka kuwa mshindi wa kusikiliza kipindi cha mkasa,kulia ni Meneja  ubunifu wa Redio 5 Vicky Mwakoyo
IMG_8938
Watangazaji wa Radio 5 wakimkabidhi mshindi wa 3 Bwana Paskal Raimond Wenga kutoka Olorien Kijenge Kapu la zawadi  ya pasaka baada ya kuibuka kuwa mshindi kwa kusikiliza vipindi vyote vya Radio 5,
Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments
Muasisi wa chama cha Tanzania Peoples Party na aliyendika chapisho la mgogoro wa mpaka wa Tanzania na Malawi  Dr. Aleck Che-Mponda, amefariki dunia leo.

Kwa mujibu wa mtoto wake Chemi Chemponda, baba yake amefariki akiwa anapata matibabu katika hospitali ya Masanna iliyopo nje kidogo ya Jiji la Dar es salaam.

Dr Che-Mponda alifanya utafiti muhimu kuhusu mgogoro katika ya Malawi na Tanzania kuhusu Ziwa Nyasa mwaka 1971 kwa ajili ya Ph.D yake kutoka Chuo Kikuu cha Howard (Howard University). Dissertation inaitwa, ''The Malawi-Tanzania Border and Territorial Disputes, 1968: A case study of Boundary and Territorial Imperatives in the new Africa". Dr. Che-Mponda alimkabidhi Mh. Balozi Manongi, nakala la andiko (dissertation) lake.  Kwa wasiofahamu, Dr. Che-Mponda ni baba yangu mzazi.


Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments
Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Simon Mwakifwamba(kulia) akielezea jambo kwa wana habari(hawapo pichani) wakati wa kutangaza walioingia katika hatua ya mwisho ya kushindania Tuzo za Filamu Tanzania leo jijini Dar es Salaam katika mkutano na wana habari uliofanyika katika hotel ya New Africa ya jijini Dar es Salaam, kulia kwake ni Mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya tuzo hizo Caroline Gul na mmoja wa wadhani kutoka International Eye Hospital Dr. Recep Yujel.
Jaji mkuu katika mchakato wa mchujo Issa Mbura kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam akitoa ufafanuzi wa vipengere 11 vilivyoainishwa kushindaniwa.
Afisa Masoko kutoka EATV/EA Radio Happy Shame ambao ni moja ya wadhamini wa tuzo hizi akitoa neno kwa niaba ya wadhamini wa Tuzo za Filamu Tanzania.
Mwakilishi kutoka Push Mobile Bwana Ezekiel akielezea namna ya upigaji kura ili kupata washindi tuzo hizi kubwa nchini.
Posted by MROKI On Tuesday, March 31, 2015 No comments

March 30, 2015

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akishiriki usafi wa mazingira katika Mtaa wa Mlalakuwa na wakazi wa Mtaa huo wakati wa operesheni maalum ya kuweka safi mazingira.
********
MPANGO wa kuweka safi mazingira ya jiji la Dar es Salaam utafanikiwa tu iwapo viongozi na watendaji watatekeleza mpango huo kwa vitendo.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam mwishoni mwa wiki wakati wa operesheni maalum ya kusafisha maeneo mbalimbali ya Kata ya Mikocheni, Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda alisema umefika wakati sasa viongozi kchukua hatua za makusudi za kuhakikisha mkakati wa kuweka safi jiji unafanikiwa kwa kuwashirikisha wananchi wao kwa vitendo.

Mwenda alithibitisha hilo kwa vitendo wakati alipojumuika na wananchi mbalimbali wa Mtaa wa Mikocheni B, Manispaa ya Kinondoni kusafisha maeneo mbalimbali ya Mtaa  huo ikiwemo sehemu za mto Mlalakuwa na kuwahakikishia wananchi wake kuwa hilo litakuwa zoezi endelevu ili kuhakikisha kila mwananchi anahamasika na kuweka safi mazingira yanayomzunguka.

“Kinondoni imekuwa Manispaa ya kuigwa katika suala la usafi, na hili tunalitekeleza kwa kujumuika na wananchi wenzangu kwa ajili ya kusafisha maeneo mbalimbali na leo tupo Kata ya Mikocheni B. viongozi wanatakiwa waoneshe wananchi wao kwa vitendo, nao watahamasika .” alisema Mwenda.


 Meya wa Manispaa ya Kinondoni akioneshwa sehemu mbalimbali za Mto Mlalakuwa wakati wakiufanyia usafi.
 Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda akiwa kwenye picha ya pamoja na wakazi wa Kata ya Mikocheni B baada ya kumaliza kufanya usafi katika mto Mlalakuwa.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (wa pili kulia) akikabidhi viroba kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Mikocheni B, Sixbert Thomas kwa ajili ya kuzuia maporomoko ya ardhi katika Mto Mlalakuwa, wakati wa operesheni hiyo.

Meya wa Manispaa ya Kinondoni, Yusuph Mwenda (kulia) akimsikiliza kwa makini Mjumbe wa Serikali ya Mtaa wa Mlalakuwa, Abraham Shoo (kushoto) wakati wa operesheni maalum ya kusafisha mazingira katika Kata za Manispaa hiyom Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Katikati ni Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa huo, Nicodemus Masika.
Posted by MROKI On Monday, March 30, 2015 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo