Nafasi Ya Matangazo

February 02, 2015





Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira James Lembeli akiwasilisha taarifa ya Utekelezaji wa Kazi za Kamati yake kwa Kipindi cha Mwaka 2014, Bungeni mjini Dodoma.

Hussein Makame-MAELEZO, Dodoma
KAMATI ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Mazingira imesema kuwa hatua za Serikali za kupambana na ujangili nchini zimeonesha mafanikio makubwa.

Akitoa taarifa ya Utekelezaji wa Kazi za Kamati, Mwenyekiti wa Kamati hiyo, James Lembeli alisema kuwa pamoja na mafanikio mengine hatua hiyo imefanikiwa kukamata silaha 2000.

Alisema hadi kufikia mwaka 2013, hali ya ujangili wa tembo ilikadiriwa kufikia tembo 30 kwa siku, lakini Serikali ilichukua hatua ya kuzuia na kutokomeza uhalifu huo kwa kuanzisha Operesheni Tokomeza.

“Pamoja na madhara yalijitokeza operesheni hiyo ilisaidia kuanza kupungua kwa kesi za ujangili wa tembo nchini” alisema Lembeli.

Alifafanua kuwa baada ya Operesheni hiyo Serikali iliendelea kuchukua hatua zaidi kwa lengo la kutokomeza kabisa tatizo hilo.

“Hatua zilizochukuliwa ni pamoja na kuajiri askari wa wanyamapori zaidi ya 500 na wengine 300 waliajiriwa ikiwa ni askari wa kujitolea”alisema.

Hata hivyo aliishauri Serikali kuendelea na harakati za kupambana kwa nguvu zote na ujangili  na kuweka wazi hali ya ujangili nchini ili wananchi na wadau wa hifadhi nchini waungane na Serikali.
Posted by MROKI On Monday, February 02, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo