Nafasi Ya Matangazo

February 11, 2015




Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chato Clement Berege pamoja na Balozi wa Japan Masaki Okada wakiweka sahihi ya msaada wa fedha kwa ajili ya mradi wa uwekwaji mashine ya kukamulia mafuta ya Alizeti, Chato. Huku Waziri wa Ujenzi ambaye pia ni Mbunge wa Chato Mhe. John Magufuli akishuhudia tukio hilo.

BALOZI wa Japan nchini Masaki Okada leo ametiliana saini na Halamashauri ya Wilaya ya chato mkoani Geita, ujenzi wa kiwanda cha kukamulia mafuta ya alizeti kitakachojengwa wilayani chato mkoani geita.


Akizungumza katika hafla hiyo balozi Okada amesema serikali ya japan imeamua kutoa msaada wa dola za Marekani 95,124 sawa na shilingi milioni 165 za Tanzania kugharamia mradi huo.



“Mradi huu ni wa kipekee katika miradi toka mfoko wa grant assistance for grassroots human security projects GGHSP kwani unalenga kuhamasisha kilimo cha alizeti wilayani chato na hivyo kuibua fursa mpya za ajira  na kuwawezesha wananchi kutumia mafuta yasio na lehemu” ,amesisitiza balozi Okada.



Akizungumza katika hafla hiyo mbunge wa chato, ambae pia ni Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli amemshukuru balozi Okada kwa misaada mbalimbali anayoitoa hapa nchini na katika jimbo la chato ili kuibua fursa za kiuchumi na  kuharakisha maendeleo.



Amewataka wajenzi wa kiwanda hicho kukijenga kwa viwango vya ubora unakubalika na kumaliza kazi hiyo kwa wakati ili kuanza uzalishaji wa mafuta kwa haraka .



“kiwanda hiki kitakapokamilika kitakuwa na uwezo wa kutengeneza lita 1600 za alizeti kwa saa moja na kukamua gunia 80 za alizeti na hivyo kuwezesha mafuta ya alizeti kusambazwa ndani na nje ya nchi na kukuza uchumi”, amefafanua waziri Dkt. Magufuli.



Naye mkurugenzi wa halamashauri ya wilaya ya chato  Clement Berege amemhakikishia balozi  kuwa msaada wa kiwanda cha kutengeneza mafuta ya alizeti utasimamiwa kikamilifu ili uwe na manufaa kwa jamii ya chato na wananchi kwa ujumla.



Katika hatua nyingine balozi Okada amesaini mkataba wa kutoa magari mawili ya kusafirisha wagonjwa ambulance katika hospitali ya taifa ya muhimbili ili kupunguza changamoto ya usafirishaji wagonjwa.



Naye kaimu mkurugenzi mtendaji wa hospitali ya taifa ya muhimbili Dkt. Hussein kidanto amemshukuru balozii wa japan kwa msaada huo wenye thamani ya shilingi milioni 70 na kuahidi hospitali hiyo iko kwenye mkakati wa kuanzisha kitengo cha ambulance ili kusafirisha kwa haraka wajawazito, wagonjwa na waathirika wa ajali na hivyo kuwafikisha katika hospitali hiyo kwa wakati.
Posted by MROKI On Wednesday, February 11, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo