Nafasi Ya Matangazo

December 09, 2014

Nyerere.
La Veda akipozi na baadhi ya wadau waliofika kumpokea.
MWANADADA, aliyeiwakilisha Tanzania katika shindano la Big Brother Hotshots, Irene Neema Vedastous ‘LA VEDA' amefunguka kuwa Diamond, Fezza na Idris wameondoa gundu kwa ushindi wao.
Akizungumza na GPL jana jioni katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, wakati akiwasili kutoka Afrika ya Kusini alipokwenda kuungana na washiriki wengine wa BBA katika fainali, La Veda alisema,
“Binafsi nimefurahi sana kwa Idris kushinda Dola za Kimarekani 300,000, ni furaha kubwa sana kwangu na kwa Watanzania kwani naamini pia Diamond kuchukua tuzo tatu za Channel O na nyingine aliyopata juzi kutoka Nigeria, Fezza kuingia tena mjengoni wote watakuwa wameondoa gundu kwa wasanii wa Kitanzania’, alisema.
Aidha La veda amewaomba Watanzani kujitokeza kwa wingi kumpokea Idris siku atakapowasili maana ushindi wake unazidi kuiweka Tanzania katika ramani nzuri kimataifa.
Posted by MROKI On Tuesday, December 09, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo