Nafasi Ya Matangazo

May 20, 2014



Waziri wa Ujenzi Dkt. John Pombe Magufuli (Mb) leo Jumanne, tarehe, 20/05/2014 anatarajiwa kuwasilisha Bajetiya Wizara ya Ujenzi bungeni kwa mwaka 2014/15.

Bajeti hiyo inayotarajiwa kuwasilishwa jioni, inayosubiriwa kwa hamu kubwa na wadau pamoja na wananchi inatarajiwa kufafanua mambo mbalimbali kuhusu sekta hiyo ya ujenzi.

Wizara ya Ujenzi ina majukumu yafuatayo, Kusimamia Sera za ujenzi na usalama barabarani, Ujenzi na matengenezo ya barabara, madaraja na vivuko.

Pamoja na majukumu hayo Wizara pia inasimamia ukarabati wa majengo ya Serikali, huduma za Ufundi na umeme, kusimamia shughuli za usajili wa Makandarasi, Wahandisi, Wabunifu Majengo na Wakadiriaji Majenzi, Usalama barabarani na mazingira katika sekta hiyo.

Pia Wizara inasimamia uboreshaji, utendaji na uendelezaji wa watumishi wa Wizara pamoja na kusimamia utekelezaji wa majukumu ya Wakala,Taasisi na Bodi zilizo chini ya Wizara.

Kwa taarifa zaidi usikose kusoma toleo la bajeti ya Wizara ya Ujenzi Kwenye tovuti ya Wizara (www.mow.go.tz) na siku ya alhamisi tarehe 22/05/2014, kwenye magazeti mbali mbali.

Posted by MROKI On Tuesday, May 20, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo