Nafasi Ya Matangazo

March 05, 2014

 Wachezaji wa timu ya taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' wakifanya mazoezi katika uwanja wa Sam Nujoma mjini Windhoek Namibia jana. Leo watashuka katika dimba hilo kuwakabili wenzao wa Namibia Brave Warriors katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki.
 Kocha msaidizi wa Taifa Stars, Hafidh Badru akizungumza na wachezaji wakati wa mazoezi.
Nahodha wa Taifa Stars, Agrey Moris akiongoza mazoezi.
*****
TIMU ya taifa Taifa Stars usiku wa leo majira ya saa 2:30 saa za Namibia, itashuka kuwakabili Brave Warriors ya Namibia katika mchezo wa kimataifa wa kirafiki.


Kikosi hicho kinachonolewa na Kocha wa mpito, Salum Madadi na Hafidh Badru kutoka Zanzibar kitawakosa nyota wake watatu wanaosakata soka la kulipwa nje ya Tanzania.


Nyota hao ni Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wanakipiga TP Mazembe ya Congo DRC  na kiungo Mwinyi Kazimoto anaekipiga Al Markhiya timu iliyopo daraja la pili mji wa  Qatari.

Baada ya mazoezi ya leo usiku katika uwanja wa Sam Nujoma, Kocha Madadi anataraji kupata kikosi cha kwanza ambachjo kitatokana na wachezaji 15 aliowasili nao jana hapa Namibia tayari kukivaa kikosi cha wachezaji wa Brave Warriors  ambacho kinadaiwa kuwa na majeruhi 3.

Madadi ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, ataunda kikosi cha kwanza kutoka kwa wachezaji Shaban Kado, Mwadin Ally, Erasto Nyoni, Abdi Hassani Banda, nahodha Agrey Moris na Said Morad.

Wengine wanaotaraji kuunda kikosi hicho ni Himid Mao, Amri Kiemba, Ramadhani Singano, Haruna Chanongo, Athanas Mdamu, Juma Luizio, Jonas Mkude na Mcha Khamis Mcha.

Msafara wa timu ya taifa unaoongozwa na Mjumbe wa Kanda ya Simiyu na Shinyanga, Epaphra Swai pamoja na kocha msaidizi Hafidh Badru, Mjumbe Ahmed Mgoi, Daktari wa timu Juma Mwankemwa, Meneja wa timu, Boniface Clemence.

Licha ya kukosa nyota hao wachezaji wameahidi ushindi mnono katika mchezo huo wa kimataifa na kulinda hadhi yao katika viwango vya soka vya FIFA.

Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, George Kavishe amesema wao kama wadhamini wanatarajia ushindi  mkubwa ili kuipandisha Tanzania katika viwango vya FIFA.

Huu ni mwaka wa pili tangu Kilimanjaro Premium Lager ianze kuidhamini Taifa Stars na imewekeza zaidi ya Dola Milioni mbili kila mwaka.
Posted by MROKI On Wednesday, March 05, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo