Nafasi Ya Matangazo

March 17, 2014


Mgombea Ubunge Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini, kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Godfrey Mgimwa  akiwa amebebwa na wafuasi wa chama hicho jana usiku katika Ofisi ya CCM Mkoa wa Iringa baada kutangazwa matokeo ya awali yasiyo rasmi .Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeibuka na ushindi wa kishindo kwa kushinda kata zote 13 zilizoko kwenye jimbo hilo la Kalenga. 
*******
Matokeo ya Uchaguzi Mdogo jimbo la Kalenga Iringa vijijini yametangazwa rasmi jana usiku na Tume ya Taifa ya Uchaguzi mjini Iringa,kuwa chama cha CCM kilipata jumla ya kura 22962,na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA),Kilipada idadi ya jumla kura 5853 na chama cha CHAUSTA kilipata kura 150.Hivyo chama cha CCM kilishinda kwa asilimia 79.4,CHADEMA asilimia 20.1 na CHAUSTA asilimia 0.5.Matokeo hayo ni ya jumla kwa Kata 13 za jimbo hilo.
 KAMANDA WA UVCCM MKOA WA IRINGA  SALIM ASAS AKICHEZA  KWA SHANGWE  VIWANJA  VYA CCM MKOA KUSHEREKEA  USHINDI  WA  CCM KALENGA

Matokeo ya Awali yasiyo rasmi baadhi ya vituo  inaongoza kwa mbali.
Posted by MROKI On Monday, March 17, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo