Nafasi Ya Matangazo

September 26, 2013


 Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt Emmanuel Nchimbi,akipata maelezo kwenye banda la Wakala wa Barabara (TANROADS) kutoka kwa Mkuu wa Kitendo cha Usalama na Mazingira,Zafarani A Mada
ni.Dkt Nchimbi alikuwa akikagua mabanda mbalimbali kabla ya kuzindua maadhimisho ya Wiki ya Usalama Barabarani yanayofanyika Jijini Mwanza Kitaifa.
  Mhandisi Rwehura wa TANROADS ,akimwonyesha Waziri wa Mambo ya Ndani,Dkt Emmanuel Nchimbi,jinsi barabara zinavyojengwa chini ya usimamizi wa Wakala huyo wa barabara.  
  Mkuu wa Kitengo cha Usalama na Mazingira wa TANROADS,Zafarani A Madai akimwonyesha Waziri wa Mambo ya Ndani Dkt Emmanuel Nchimbi,jinsi madereva wanavyopaswa kutumia barabara ili kuepusha ajali kwa kutumia michoro mbalimbali . 
 Mhandisi wa TANROADS Jonas Matete, akiwapa maelekezo ya matumizi ya barabara vijana wawili ambao walitembelea banda la wakala huyo wa barabara ili kufahamu mambo mbalimbali wakati wa maadhimisho ya Wiki ya Usalama Barabarani yanayofanyika jijini Mwanza. Picha na Aisha Malima
Posted by MROKI On Thursday, September 26, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo