Nafasi Ya Matangazo

July 17, 2013

Mkurugenzi wa Tan Communication Media  inayo miliki kituo cha  Radio 5 chenye makao yake makuu jijini Arusha  Bw Robert Francis (kulia) akimkabidhi Pikipiki Mfanyakazi Bora wa Kituo hicho Semiyo Sonyo.
 **********
Mkurugenzi wa Tan Communication Media  inayo miliki kituo cha  Radio 5 chenye makao yake makuu jijini Arusha  Bw Robert Francis Amewataka watangazaji na wanahabari wanaofanya kazi katika vituo vya Radio na Televisheni hapa nchini kuzingatia weledi wa kitaaluma wanapofanya shughuli zao za kila siku ili kusaidia jamii ya kitanzania kukabiliana na changamoto katika kipindi hiki ambacho dunia inabebwa na utandawazi. 
Akikabidhi pikipiki kwa mtangazaji bora wa kipindi cha usiku cha LOVE CUTTS kinacho rushwa Radio 5 katika Hafla fupi iliyofanyika jijini Arusha, Mkurugenzi Robert amesema vyombo vya habari vya kielectonic yaani Televisheni,Radio, na mitandao ya kijamii vinafikia watu kwa haraka zaidi na kwa unafuu wa gharama kuliko machapisho na kwamba vikitumika bila miiko ,weledi na kuzingatia kanuni za kitaaluma vinaweza kuwa sehemu ya tatizo badala ya kuwa vyombo vya kusukuma kasi ya maendeleo.
 
Katika tafrija hiyo Mtangazaji Semio Sonyo amekabidhiwa pikipiki ikiwa ni sehemu ya motisha zinazo tolewa na kituo cha Radio five kwa wafanyakazi
wake waofanya vizuri katika majukumu yao.
Semio Sonyo akijaribu pikipiki aliyokabidhiwa na mkurugenzi wa Tan Communication Media,bwana Robert Francis
Posted by MROKI On Wednesday, July 17, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo