Nafasi Ya Matangazo

March 19, 2013



WACHEZAJI wa Kimataifa wa Tanzania wanaocheza Soka la Kulipwa Nchini Congo DRC, wanaochezea timu ya TP Mazembe Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu wamewasili nchini jana na kuwahakikishia Watanzania Ushindi dhidi ya Morocco.

Samata na Ulimwengu wamewasili nchini wakitokea Nchini Boswana walikokuwa na Timu yao ya TP Mazembe na kuja kuungana na wenzao katika Kambi ya Timu ya Taifa inayo jinoa dhidi ya Morocco mchezo utakao fanyika baade mwezi huu.

Akizungumza mara baada ya kuwasili, Mbwana Samata amesema ushindi dhidi ya Morocco ni lazima, hivyo Watanzania wasiwe na hofu na timu yao na wao wako tayari kuliongoza jahazi hilo la ushindi.

“Tumekuja kuungana na wachezaji wenzetu wa Timu ya Taifa, tumekuja kuhakikisha timu yetu inashinda na tuna kila sababu ya kushinda maana tunacheza Nyumbani,” alisema Samata.


Amesema kuwa wao wako fiti na hawana tatizo lolote na wanajiunga na kambi usiku huo huo waliowasili na kuanza mazoezi kama ratiba ilivyo pangwa na hivyo watanzania wajiandae kushangilia ushindi.

Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro lager, imeingia kambini tangu juzi kujiandaa na mchezo huo dhidi ya Morocco jijini Dar es Salaam.

Taifa Stars itacheza mechi ya mchujo kuwania tiketi ya kucheza Fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil dhidi ya Morocco. Mechi hiyo itachezwa Jumapili Machi 24, katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaocheza soka la Kulipwa nchini Congo DRC katika Timu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu (kushoto) na Mbwana Samata wakiwa uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam mara baada ya kuwasili tayari kwa kujiunga na kambi ya Timu ya Taifa ikiwa ni maandalizi ya kuikabili Morocco.

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaocheza soka la Kulipwa nchini Congo DRC katika Timu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu (kushoto) na Mbwana Samata wakizungumza na mmoja wa mashabiki wa Soka nchini Tanzania aliyewalaki walipo wasili  uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana tayari kwa kujiunga na kambi ya Timu ya Taifa ikiwa ni maandalizi ya kuikabili Morocco.

Wachezaji wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, wanaocheza soka la Kulipwa nchini Congo DRC katika Timu ya TP Mazembe, Thomas Ulimwengu (kulia) na Mbwana Samata wakizungumza na mmoja wa Mfanyakazi wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Haji Mpangachuma (katikati) aliyewalaki walipo wasili  uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam jana tayari kwa kujiunga na kambi ya Timu ya Taifa ikiwa ni maandalizi ya kuikabili Morocco.
Posted by MROKI On Tuesday, March 19, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo