Nafasi Ya Matangazo

March 13, 2013

Papa Francis
Hatimae Jopo la Makardinali 115 wa Kanisa katoliki wamemchagua Kardinali wa Buenos Aires kutoka Latin Amerika Jorge Mario Bergoglio (76) kuwa kiongozi mpya atakaye chukuwa nafasi ya  Papa Benedict aliyejiuzuli hivi karibuni.

Jorge Mario Bergoglio ambaye ni Muagrgentina tayari amechagua jina la atakalo litumia katikakipindi chake cha Uongozi kuwa atatambulika kama Papa Francis.

Jopo la Makardinali wamemchagua Cardinali kutoka Latin America Cardinal Jorge Mario Bergoglio, kushika wadhifa mpya wa  Papa katika uchaguzi uliofanyika kwa mara ya tano kwa kura zilizopugwa na Makadinali 115 waliokuwa wakikutana katika kanisa la Sistine Chapel huko Vatican , Roma.

Maelfu ya watu walikuwa wamefurika katika eneo la la St. Peters huko Vatican huku mamilioni wengine wakishuhudia Papa huyo mpya akitangzawa mbele yao.


Papa Francis ni Papa wa Kwanza kuchaguliwa kutoka Latin America tangu kuanzishwa kwa Kanisa Katoliki Duniani.
Aliwahi pia kutajwa kumrithi Papa John Paul II wakati wa kumtafuta Papa na akashinda Papa Benedict ambaye amejiuzulu.

Posted by MROKI On Wednesday, March 13, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo