Nafasi Ya Matangazo

October 16, 2012

 
Michezo ya Bandari maarufu kama ‘inter-ports games’ imeanza rasmi katika viwanja vya CCM Kirumba jijini Mwanza ambapo mashabiki wameonesha kuridhishwa na michezo ya awali ya ufunguzi huku wachezaji wakionesha vipaji vya hali yajuu katika michezo ya soka, mpira wa kikapu, pete na kuvuta kamba.

Michezo hiyo ambayo imefunguliwa na Naibu Waziri wa Uchukuzi, Dk. Charles Tizeba (MB),aliyefurahishwa na kuridhishwa na maandalizi yake, inategemewa kufanyika kwa muda wa siku tano kuanzia Agosti 15 katika jiji la Mwanza.

Dk. Tizeba amewaasa wachezaji kucheza kwa upendo na staha na kukumbuka kwamba michezo inajenga undugu na mshikamano na si uadui. Aidha amewakumbusha wachezaji kuendelea kushiriki katika michezo mbalimbali kwa ajili ya kuboresha afya zao mara baada ya kukamilka kwa michezo hii.

Michezo ya ‘inter-ports games’ inazikutanisha bandari za Dar es Salaam, Tanga, Mtwara, Mwanza, Kyela, Kigoma na Makao Makuu ambapo michezo ya mpira wa miguu, kuvuta kamba, bao, riadha, kikapu na mprira wa pete itashindaniwa.
 Mchezo wa Bao nao upo na hapa wakichuana
 Wanaume wa shoka wa mchezo wa kuvuta kamba kutoka Dar es Salaam port wakiwania ushindi.
Mashabiki wakifuatilia michezo hiyo ndi ya uwanja wa Kirumba jijini Mwanza.
Posted by MROKI On Tuesday, October 16, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo