Nafasi Ya Matangazo

August 09, 2011

Watoto wa Shule mbalimbali za msingi wakiandamana katika sherehe za uzinduzi wa ripoti ya Utafiti na Mpango wa Kitaifa wa kushughulikia "Ukatili kwa Watoto" na mpango wa Udhibiti wa Taifa.
Katikati ni Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Umoja Mataifa Bi. Asha Rose Migiro,  wa pili kushoto ni Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto Mh. Sophia Simba, wa kwanza kushoto Waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi Dkt. Shukuru Kawambwa, wa Pili Kulia ni Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI (Elimu) Bw. Majaliwa Majaaliwa na wa Kwanza Kulia ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Haji Mponda kwa pamoja wakikaribishwa maandamano yaliyokuwa yakiingia katika viwanja vya Karimjee.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bi. Asha Rose Migiro akizungumzia umuhimu wa Taifa kusimamia haki ya mtoto ya kuishi kwa amani na furaha bila kufanyiwa Ukatilii wa aina yoyote katika Kilele cha uzinduzi wa ripoti ya Utafiti na Mpango wa Kitaifa wa kushughulikia "Ukatili kwa Watoto" na mpango wa Udhibiti wa Taifa.
Mabalozi wawakilishi wa nchi mbalimbali nchini wakifuatilia uzinduzi wa ripoti hiyo.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Taifa Dkt. Asha Rose Migiro na Waziri wa Maendeleo ya jamii, Jinsia na Watoto Mh. Sophia Simba wakizindua rasmi RIPOTI YA UTAFITI NA MPANGO WA KITAIFA WA KUSHUGHULIKIA "UKATILI KWA WATOTO" NA MPANGO WA UDHIBITI WA TAIFA.
Posted by MROKI On Tuesday, August 09, 2011 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo