Nafasi Ya Matangazo

July 15, 2011

Mzee Yusuf na Juma nature kutumbuiza tamasha kubwa la Epiq Nation kwenye viwanja vya Mwembeyanga Temeke kesho Jumamosi.
Meneja wa Mradi wa Epiq Nation wa kampuni ya Zantel, Deogratius Ringia akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu tamasha kubwa la 'Epiq Nation' litakalofanyika kesho Jumamosi kwenye viwanja vya Mwembe Yanga Temeke ambapo wasanii Mzee Yusuf (kushoto) wa kundi la Jahazi Modern Taarab na Juma Kassim 'Sir Nature'  (kulia) wa kundi la TMK Wanaume Halisi watatumbuiza.
Kiongozi wa kundi la TMK Wanaume  Halisi, Juma Kassim 'Sir Nature'  (kulia) akieleza kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu ushiriki wa kundi lake katika tamasha kubwa la Zantel  Epiq Nation litakalofanyika kesho Jumamosi kwenye viwanja vya Mwembe Yanga Temeke. Kushoto ni Kiongozi wa kundi lingine litakaloshiriki la Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf  na Meneja wa Mradi wa Epiq Nation, Deogratius Ringia.
Kiongozi wa kundi la Jahazi Modern Taarab, Mzee Yusuf  akieleza kwa waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana kuhusu ushiriki wa kundi lake katika tamasha kubwa la Zantel  Epiq Nation litakalofanyika kesho Jumamosi kwenye viwanja vya Mwembe Yanga Temeke. Kulia ni Kiongozi wa kundi lingine litakaloshiriki la TMK Wanaume  Halisi, Juma Kassim 'Sir Nature' na Meneja wa Mradi wa Epiq Nation, Deogratius Ringia.
Posted by MROKI On Friday, July 15, 2011 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo