Mgombea Ubunge wa Singida mjini kupitia chama cha CCM, Mohamed Dewji leo amemalizia ziara ya kampeni katika Kijiji cha Mtamaa A kwa kutembelea gulio la kila wiki la Mtamaa na kuzungumza na watu pamoja na kutembelea katika makazi. Pichani akimbusu mmoja wa wakina mama waliompa baraka za ushindi.
Picha hizi akitoka katika nyumba za wakazi wa Mtamaa A
Hapa akiingia katika nyumba hizo leo.
Alivutiwa na ufinyanzi wa akina mama wa Jimbo lake na kuwataka kuanzisha vikundi vya ushirika ili iwe rahisi kuwasaidia.
salamu hakubagua
Vijana nao alizungumza nao na kuwasihi kuanzisha vikundi maana si rahisi kumsaidia kijana moja mmoja. Jioni hii atahitimisha kampebni hizo katika Uwanja wa Namfua mjini Singida.




hivi huyo mo haoini aibu kutoka ktika vimbo hivyo na kuonesha namna gani hali ya wapiga kura wake ilivyo na tulivyokuwa wajinga bado tunaendelea kumpa kura watanzania tutakuwa wajinga hadi lini
ReplyDeleteYaani mimi naona kama this pose is for the camera.. ni mchezo wa kuigiza.. maana ningeziona picha kama hizi wakati si wa kuomba kura ineonesha kweli anajali.. pia hizo nyumba inaonesha hali mbaya ya maisha, katika miaka 5 iliyopita amefanya nini kupunguza umaskini? iweje leo ahamasishe waunde vikundi wakati angeshahamasisha kwa miaka 5 iliyopita? jamani wanasiasa kuweni serious basi..
ReplyDeletehuna lolote we somji kemcho na kuwaamkia waamkie
ReplyDelete