Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akisalimiana na mafundi na wahandisi wa Kichina wanaojenga jengo la mapokezi la viongozi na watu mashuhuri kwenye uwanja wa dege wa Julius Nyerere May 2, 2010 ambalo litatumika katika mapokezi ya viongozi watakaowasili nchini kuhudhuruia mkutano wa World Economic Forum unaotarajiwa kuanza kwenye ukumbi wa Mlimani City jijini Dar e salaam, May 5, 2010.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akikagua maandalizi ya mapokezi ya viongozi wakuu wa n chi mbalimbali na washiriki wa Mkutano wa World Economic Forum kwenye uwanja wa ndege wa Julius Nyerere May 2, 2010. Mheshimiwa Pinda pia alikagua ukumbi wa Mlimani City utakapofanyika mkutano huo.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akizungumza na Waandishi wa Habari May 2, 2010 baada ya kukagua maadalizi ya mapokezi ya wageni watakaoshiriki katika Mkutano wa World Economic Forum unaotarajiwa kufanyika jijini Dar es salaam kuanz a May 5, 2010 kwenye ukumbi wa Mlimani City utakapofanyia mkutano huo. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu, Peniel Lymo na kushoto ni Mkurugenzi wa Afrika wa World Economic Forum, Catherine Tweedie.
Posted by MROKI
On Sunday, May 02, 2010
1 comment
INASIKITISHA TZ HATA SEHEMU YA KUPOLKELEA TU WAGENI KUIJENGA INAHITAJI MKANDARASI WA NJE WAKWETU WAKOWAPI?
ReplyDelete