Nafasi Ya Matangazo

November 04, 2009

EVELYNE ashinda tuzo ya Miss National Costume

Mshindi wa pili wa Miss Universe Tanzania Evelyne Amasi ambaye anashikilia taji la Miss Earth Tanzania 2009, ameshinda tuzo ya Miss National Costume.


Mashindano ya Miss Earth ambayo yanafanyika tangu Novemba mosi mpaka 22 mwaka huu, huko nchini Philippines, Evelyne Amasi (23), mrembo ambaye ameondoka nchini mwishoni mwa mwezi wa kumi kwenda kuiwakilisha Tanzania katika mashindano ya kumtafuta Miss Earth, ameshinda tuzo ya vazi la taifa (National costume) katika mashindano ambayo yalishirikisha zaidi ya warembo 80 kutoka nchi mbali mbali duniani kote.


Evelyne ambaye aliondoka nchini mwanzoni mwa mwezi huu( Oktoba 31), alifanikiwa kushinda tuzo ya Miss National Costume 2009 na kutwaa nishani na pesa taslimu ambayo atakuja kupewa siku ya fainali.

Ushindi wa Mrembo huyu, ulikubaliwa na wengi kutokana na uzuri na uasili wa mavazi ya mrembo huyu.

Mavazi ya mwanadada huyu yalikuwa tofauti na mavazi ya warembo wengine kwani zilikuwa zimetengenezwa kwa kutumia kambakamba zilizotokana na magome ya miti ambazo zimesukwa kwa ustadi na kuwakilisha vyema matumizi halisi ya mazingira yetu.

Mbali ya vazi hilo ambalo lilionekana kama kichaka cha mti vilevile kulikuwa na nyoka aliyetengenezwa kwa ubunifu wa hali ya juu na juu kichwani kulikuwa na kilemba ambacho kimetumika kama kichaka cha ndege anachotagia mayai yake. Nguo hiyo ilibuniwa na mbunifu chipkizi Diana Magese toka mkoani Morogoro.


Katika kinyanganyiro hicho Evelyne ndio alikuwa mshindi wa kwanza kushinda tuzo hiyo akifuatiwa na mrembo toka Puerto Rico na Miss Guam.

Katika mashindano haya, washindi wanaofanikiwa kushinda tuzo ndogondogo ndio wenye nafasi kubwa ya kuingia nusu fainali yaani top Sixteen(16 bora)
Mwaka jana Tanzania iliwakilishwa na mrembo Miriam Odemba na kufanikiwa kuitangaza vyema nchi yetu kwa kuingia katika kumi na tano bora ya mavazi ya ufukweni na vazi la Taifa katika mashindano madogo na hatimaye kushika nafasi ya pili katika fainali na kutwaa taji la Miss Earth Air-2008, ambapo mshindi wa kwanza alitoka nchini Phillipines.

Fainali za mashindano ya Miss Earth mwaka huu yatafanyika tarehe 22 mwezi wa kumi na moja huko Boracay Island nchini Philippines.
Posted by MROKI On Wednesday, November 04, 2009 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo