Nafasi Ya Matangazo

May 31, 2009

Mwandaaji wa Miss Universe, Maria Sarungi akimvika taji la ushindi mrembo kutoka Mwanza, Illuminata James.Wanyange walioingia hatua ya kumi bora.
Wageni waalikwa wakifuatilia shindano...
Wasindi watatu bora wakiwa na Miss Universe 2009, Illuminata James (katikati) baada ya kuvikwa taji lake. Kungwi wa warembo Miriam Odemba (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Miss Universe na mama wa mrembo huyo.
Hawa ni Diamond Musica wakishambulia jukwaa.
Huyu nae kutoka Kenya, mwadada WAHU alipagawisha wageni kwa mapigo yake na umahiri wa kuimba.




Posted by MROKI On Sunday, May 31, 2009 1 comment

May 29, 2009

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dk. Ali Mohamed Shein, akiwasha Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa CCM Kirumba mjini Mwanza leo kwa ajili ya kukimbizwa katika Mkoa yote ya Tanzania ambapo jumla ya miradi 138 itakayoharimu jumla ya shilingi 8.6 Bilion itazinduliwa katika mbio za Mwenge mwaka huu, ujumbe wa mwaka huu ni pinga ukatili wa kijinsia wa watoto na Albino. Kulia ni waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Prof Juma Kapuya.
Posted by MROKI On Friday, May 29, 2009 No comments
Baadhi ya warembo watakaoshiriki shindano la Miss Universe 2009
wakipozi kwa picha walipotembelea Kijiji cha makumbusho, Dar es
Salaam jana. Shindano hilo linatarajiwa kufanyika Mei 30,2009 katika Ukumbi wa
Mlimani City Conference Jijiji Dar es Salaam.
Baadhi ya warembo watakaoshiriki shindano la Miss Universe 2009
waklicheza ngoma ya asili ya kusini mwa Tanzania walipotembelea Kijiji
cha makumbusho, Dar es Salaam jana. Baadhi ya warembo watakaoshiriki shindano la Miss Universe 2009
wakipozi kwa picha na Kaimu Mkurugenzi wa Bodi ya Utalii Tanzania,
Geofrey Meena (katikati) walipotembelea ofisi za TTB, Dar es Salaamjana.
Mmoja wa majaji watakaoshiriki katika kinyang’anyiro cha kumtafuta
Miss Universe 2009, Roise Motene kutoka Afrika Kusini akiwasili katika
Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, Dar es Salaam juzi.
Posted by MROKI On Friday, May 29, 2009 No comments

May 27, 2009

Mrema akiwa na vijana katika kijiwe cha kuuzia magazeti na wauza fremu za picha Samora.
Mrema akisoma gazeti wakati akisubiri kupatiwa betri mpya ya simu.
Mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema akisalimiana na vijana wanaofanya shughuli zo katika mtaa wa Samora Dar es Salaam jana alipofika kutafuta mahitaji yake. Mrema aliwaambia vijana hao kuwa kwa sasa hana nia ya kuwania urais tena na sasa anarudi likizo kijijini kwao na kujipanga kuwania Ubunge ili akateme cheche Bungeni.
Posted by MROKI On Wednesday, May 27, 2009 No comments






Mtakao penda vitu hivyo msisite kuwasiliana nae.
Posted by MROKI On Wednesday, May 27, 2009 2 comments

May 25, 2009

Mgombea wa CCM Lolesia Bukwimba akishangilia baada ya kutangazwa rasmi kuwa Mbunge wa Jimbo pa Busanda wilayani Geita katika uchaguzi mdogo uliofanyika Jumapili baada ya kupata kura 29242 dhidi ya 22799 za Mgombea wa CHADEMA Finias Magesa.
Baadhi ya wafuasi wakishangilia muda mfupi baada ya mgombea wao kutangazwa mshindi wa jimbo la Busanda wilayani Geita.
Aliyekuwa mgombea wa CHADEMA katika jimbo la Busanda Finias Magesa (kulia) akimueleza jambo Mwenyekiti wa Taifa wa chama hicho(kulia) usiku mara baada ya kupata matokeo kwamba chama chao kimeshindwa kwenye uchaguzi huo.
Mamia ya wafuasi wa CHADEMA katika mji mdogo wa katoro wakishangilia baada ya kupata matokeo ya awali ya uchaguzi wa jimbo la Busanda kwamba wameishinda CCM katika kata ya Katoro kwa kupata kura 3565 dhidi ya 2757 za CCM,hata hivyo nderemo hizo zilizimika jana baada ya matokeo ya jumla kuonyesha kwamba CCM imeshinda katika jimbo hilo.
Posted by MROKI On Monday, May 25, 2009 No comments
Washiriki 20 wa shindano la Miss Universe Tanzania 2009 wakipozi kwapicha mbele ya waandishi wa bahari katika Hoteli ya Belinda, Dar esSalaam jana wakati wa uzinduzi wa kambi yao ya maandalizi ya shindanohilo linalotarajiwa kufanyika Mei 30 mkwa huu katika Ukumbi wa MlimaniConference Centre jijini humo.
Posted by MROKI On Monday, May 25, 2009 No comments
CHAMA CHA MAPINDUZI KIMESHINDA KATIKA UCHAGUZI MDOGO WA UBUNGE KATIKA JIMBO LA BUSANDA.
Posted by MROKI On Monday, May 25, 2009 No comments

Golikipa maarufu nchini Juma Kaseja akiwa mbele ya gari jipya aina ya DODGE na Nissan Munarano (juu) lililozinduliwa jana na Kampuni ya kuuza magarti ya DT Dobie Dar es Salaam jana.
Posted by MROKI On Monday, May 25, 2009 No comments

May 24, 2009

Mke wa Rais Salma Kikwete akihutubia wakati wa uzinduzi wa harambee ya kuchangisha fedaha kwaajili ya Watoto walemavu iliyoandaliwa na Mfuko wa Elimu Tanzania Dar es Salaam jana. Mke wa Rais Salama Kikwete akimkabidhi cheti cha shukrani kwa Afisa Uhusiano Mkuu wa Shirika la Nyumba Tanzania (NHC) Muungano Saguya baada ya NHC kuchangia sh milioni 11..5 katika harambee ya kuchangua mfuko wa Elimu Tanzania(TEA) kwa watoto wenye ulemavu Dar es Salaam jana.
Warembo waliowahi kushinda taji la Miss Tanzania miaka ya nyuma wakiwa katika picha ya Pamoja jana baada ya kuonyesha mavazi ambayo yatanadiwa kwaajili ya kuchangia fedha kwa watoto walemavu yaliyoandaliwa na Mfuko wa Elimu Tanzania jana.
Posted by MROKI On Sunday, May 24, 2009 1 comment
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, Dulayo bongo flava Juma Nature ‘SirNature’ akiimba wakati akisindikiza utambulisho wa albamu ya JumaNature ya ‘ Tugawane Umasikini’ katika ukumbi wa Da West Park InnTabat, Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Tigo ilidhamini onyesho hilo.
Msanii mahiri wa muziki wa bongo flava Juma Nature ‘Sir Nature’akipagaisha mashabiki wake wakati akiitambulisha albamu yake ya ‘Tugawane Umasikini’ katika ukumbi wa Da West Park Inn Tabata, Dar esSalaam mwishoni mwa wiki. Onyesho hilo lilidhamini wa na Tigo.
Msanii wa muziki wa kizazi kipya, PMC, akilitawala jukwaa wakatiakisindikiza utambulisho wa albamu ya Juma Nature ya ‘ TugawaneUmasikini’ katika ukumbi wa Da West Park Inn Tabata, Dar es Salaammwishoni mwa wiki. Tigo ilidhamini onyesho hilo.
Msanii wa miondoko ya Hip Hop, O Ten akifanya vitu vyake wakati wautambuilisho wa albamu mpya ya Jumas Nature ya Tugawane Umasikinikatika Ukumbi wa Da West Park Inn, Tabata jijini Dar es Salaammwishoni mwa wiki. Utambulisho huo ulidhamniwa na Tigo.
Posted by MROKI On Sunday, May 24, 2009 No comments
Wabinifu wa mitindo mbalimbali ya mavazi Hadija Mwanamboka na Musatafa Hassanali wakiwa katika pozi wakati wa harambee ya kuchangia fedha kwaajili ya watoto walemavu usiku wa kuamkia leo Dar es Salaam.
Posted by MROKI On Sunday, May 24, 2009 No comments
Event: Miss Universe Tanzania 2009 finals

"Be there ... there is no repetition.....this is the real deal!"

What: Ceremony

Host: Miss Universe Tanzania 2009

Start Time: Saturday, May 30 at 7:30pm
End Time: Saturday, May 30 at 11:30pm

Where: Mlimani City Conference Center

Posted by MROKI On Sunday, May 24, 2009 No comments

May 23, 2009

Waziri wa Fedha na Uchumi, Mustafa Mkulo 9katikati) akimkabidhi hundi ya gawio ya sh milioni 870 kwa mmoja wa wanahisa wa Benki ya NMB, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya Exim Sabetha Mwambenja, kwaniaba ya Benki hiyo jana wakati wa kugawa gawio kwa wanahisa. Kulia nai Mwenyekiti wa Bodi ya NMB, Misheck Ngatunga.
Posted by MROKI On Saturday, May 23, 2009 No comments
Event: AFRICA FASHION WEEK 2009 "MUSTAFA HASSANALI TANZANIA Showcase"What: PerformanceHost: Mustafa Hassanali Couture and Concepts
Start Time: Sunday, June 14 at 6:00pmEnd Time: Sunday, June 14 at 6:30pm
Where: PAVILION ROOM, SANDTON CONVENTION CENTRE
Posted by MROKI On Saturday, May 23, 2009 No comments

May 22, 2009

Rais Bingu wa Mutharika akila kiapo cha kuitumikia Malawi kwa awamu nyingine ya miaka mitano mbele ya Jaji Mkuu wa Nchi hiyo Lovemore Munlo baada ya kushinda kwenye uchaguzi mkuu uliofanyika hivi karibuni nchini Malawi.
Makamu wa Rais Dk Ali Mohamed Shein akijadiliana jambo na Jaji Mkuu wa Malwi Lovemore Munlo katika uwanja wa Kamuzu kabla ya jaji huyo kumwapisha Dk Bingu wa Mutharika kuwa Rais wa malawi kwa awamu nyingine ya miaka mitano.
Rais Bingu wa Mutharika akimsalimia Mke wa Makamu wa Rais Mwanamwema Shein jan. Katikati i Makamu wa Ris Dk. Ali Mohamed Shein.
Posted by MROKI On Friday, May 22, 2009 1 comment
Mke wa RaisSalma Kikwete akiwa na mbunge wa Kyela Dr. Harrison Mwakyembe jana alipo mtembelea na kumjulia hali katika hospitali ya Muhimbili (MOI), Alipolazwa baada ya kupata ajali ya gari huko Iringa.
Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimfariji Mbunge wa Kyela, Harison Mwakyembe jana ambayae amelazwa katika Taasisi ya Mifupa ya Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kufuatia ajali ya gari aliyopata mkoani Iringa.
Posted by MROKI On Friday, May 22, 2009 No comments
Rais Jakaya Kikwete wa Tanzania ameweka rekodi ya kuwa rais wa kwanza wa Afrika kukutana na Rais wa Marekani Barak Obama katika Ikulu yake nchini Marekani. Rais Kikwete amekutana na mwenyeji wake huyo jana wakati wa ziara yake ya siku tisa ya kiserikali kuitembelea nchi hiyo.
Posted by MROKI On Friday, May 22, 2009 No comments

May 21, 2009

Rais Jakaya Kikwete akizungumza na Mcheza Filamu wa Marekani Steven Seagal wakati watafrija iliyoandaliwa na Madaktari wa Kimarekani kwaajili ya Afrika mjini Los Angels ambapo rais Kikwete alitunukiwa tuzo kwa jitihada zake za kuimarisha huduma za afya nchini. Seagal pia ni mwandishi wa miziki na Mtengenezaji wa filamu.
Posted by MROKI On Thursday, May 21, 2009 No comments
Mbunge wa Kyela Dk. Harrison Mwakyembe akiingizwa katika gari la wagonjwa la kampuni ya Ultimate baada ya kupokelewa katika uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalimu Nyerere Dar es Salaam leo akitokea Iringa alipo patia ajali ya gari na kupelekwa Taasisi ya Mifupa Muhimbili (MOI) kwa matibabu.
Ndege ya Kukodi ya Tanzaair 5H TZT iliyombeba kamnada.

Marafiki wa Mwakyembe walishikwa na simanzi.
Posted by MROKI On Thursday, May 21, 2009 1 comment
Wakati Maelfu ya wakazi wa Dar es Salaam wakiwa hawajapona jeraha la DECI, Wakazi wa Ukonga na maeneo ya Jirani nao walio kuwa wakipanda mbegu katika taaisia ya Malingumu Investiment walifurika jana kudai fedha zao walizokuwa wakipanda kwa kuahidiwa kupewa mikopo kuingia mitini.
Posted by MROKI On Thursday, May 21, 2009 3 comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo