Nafasi Ya Matangazo

March 23, 2015

 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiangalia bwawa la maji kwa ajili ya umagiliaji kijiji cha Kishisa  ambalo lina uwezo wa kubeba lita 5,520,000,likiwa na uwezo wa kumwagilia hekta 200 na linanufaisha kaya 696.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akisalimiana na Kaimu Mganga Mfawidhi wa hospitali ya wilaya ya Siha Dk.Loveland Makundi
 Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri akimuelezea Katibu Mkuu wa CCM namna ambavyo jimbo lake linaboresha huduma za afya.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akitoka kukagua maabara ya kisasa ya hospitali ya wilaya ya Siha,kulia ni Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri

 Hospitali ya wilaya ya Siha.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wananchi wa wilaya ya Siha kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye uwanja wa CCM wilaya ambapo alisisitiza CCM itaendelea kutetea haki za wanyonge.
 Wananchi wa wilaya ya Siha wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana huku wakinyeshewa na mvua mvua
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana (kushoto) akifurahia jambo pamoja na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Siha Ndugu Oscar Jeremia Temi na MNEC wa wilaya ya Siha wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kwenye uwanja wa CCM wilaya ya Siha.
 Mbunge wa Jimbo la Siha na Naibu Waziri wa TAMISEMI Ndugu Aggrey Mwanri akihutubia wakazi wa wilaya ya Siha kwenye mkutano wa hadhara ambao mgeni wa heshima alikuwa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana.
 Wananchi wakifuatilia mkutano
 Mbunge wa Viti Maalum Betty Machangu akihutubia wananchi na kuwaambia wajiandikishe kwenye daftari la kudumu la wapiga kura kwani ndio fursa pekee ya wao kupiga kura wakati Katiba na chaguzi zingine za Serikali.

 Wasanii wa Kimaasai wakiimba mbele ya Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana
 Sehemu ya umati wa watu
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipanda mti mara baada ya kuifungua ofisi ya CCM wilaya ya Siha.
 Katibu wa NEC Itikadi na Uenezi Nape Nnauye akisalimia wananchi wakati wa ufunguzi wa ofisi ya CCM wilaya.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akikata utepe kama ishara ya kufungua ofisi ya CCM wilaya ya Siha.( Picha na Adam Mzee)
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Posted by MROKI On Monday, March 23, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo