Nafasi Ya Matangazo

December 22, 2014

Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam leo katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Said Meck Sadik na kulia ni katibu wa Baraza la wazee wa Dar es Salaam Mzee Mtulia.

 Rais Jakaya Kiwete akihutubia taifa hii leo katika ukumbi wa Diamond Jubelee jijini Dar es Salaam kupitia wazee wa jiji hilo. 

Pampoja na mambo mbalimbali Rais Kikwete amezungumzia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika nchini kote na kuunga mkono maamuzi ya Waziri TAMISEMI, Hawa Ghasia juu ya maamuzi ya kuwatimua kazi, kusimamisha, kuwashusha vyema na kuwapa maonyo ya madaraja mbalimbali watendaji wote waliohusika na kuharibika kwa uchaguzi huo katika maeneo yao.

Rais Kikwete hivi sasa anazungumzia sakata la ESCROW ambapo kwa mambo kadhaa ambayo yalikuwa yakisubiri uamuzi wake ikiwa ni pamoja na kuwaondoa mawaziri tajwa.


Rais Kikwete amesema Mwanasheria Mkuu wa Serikali  tayari amejiuzulu, Bodi ya Tanesco imeshamaliza muda wake na tayari amesha teua Mwenyekiti Mpya wa Bodi huku Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka akisema amesha zungumza nae na amemuomba apishe nafasi yake ateuliwe mtu mwingine.

Upande wa Waziri wa Nishati na Madini, Prof. Sospeter Muhongo ameomba amuweke kiporo yeye na Katibu Mkuu wake, Eliakim Maswi kupisha uchunguzi dhidi yao. 
 
Baadhi ya wazee na wananchi wakimsikiliza kwa makini Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete wakati alipokuwa akilihutubia taifa kupitia wazee wa Dar es Salaam katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam leo.
11
Wanahabari wakichukua kumbukumbu kwenye mkutano huo wa Mh.Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na taifa kupitia Wazee wa Dar es Salaam leo  Desemba 22, 2014 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Bofya Link hiyo kumsikiliza 
Posted by MROKI On Monday, December 22, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo