Nafasi Ya Matangazo

June 14, 2025





Na Mwandishi wetu, Ruangwa, Lindi
Naibu Waziri wa Madini Dkt. Steven Kiruswa amesema kuwa, maendeleo ya Sekta ya Madini yanapelekea kuwa kitovu cha uchumi nchini, hii ni kutokana na mageuzi mbalimbali yanayoendelea kufanyika.

Dkt. Kiruswa ameyasema hayo leo Juni 13, 2025, wakati akizungumza na vyombo vya habari mapema baada ya kutembelea mabanda katika maonesho ya madini yanayoendelea kufanyika  wilayani Ruangwa.  

Akielezea kuhusu uwekezaji wa ndani Dkt. Kiruswa ameeleza kuwa, Tanzania imekuwa kivutio kikubwa  cha wawekezaji katika Sekta ya Madini kutokana na utajiri wake wa madini mbalimbali yakiwemo madini ya kinywe, makaa ya mawe pamoja na madini adimu na madini mkakati.

Kuhusu kukua kwa Sekta ya Madini, Dkt. Kiruswa amebainisha kuwa, Sekta hii imeendelea kukua kwa kasi  ambapo kwa sasa inachangia asilimia 10.1 kwenye Pato la Taifa.

Dkt. Kiruswa ameongeza kuwa, ukuaji huu unatokana na mipango endelevu hususan katika  uongezaji thamani madini, uwekezaji wa mitaji ya ndani na ya nje pamoja na Sera madhubuti za  usimamizi wa rasilimali madini nchini.

Pamoja na mambo mengine, Serikali imeendelea kusisitiza  kuhusu uongezaji thamani madini kufanyika ndani ya nchi kabla ya kusafirishwa nje ya nchi, ujenzi wa viwanda vya kusafisha dhahabu, ujenzi wa maabara za uchenjuaji na uchakataji madini.

*# MineralValueAddition*
*#GDP:10.1%FromMineralSector*
*#Vision2030:MadiniNiMaishaNaUtajiri*
Posted by MROKI On Saturday, June 14, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo