Nafasi Ya Matangazo

April 29, 2025

 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, uteuzi huo ni kama ifuatavyo:-
 
Arch Dkt. Fatma Kassim Mohamed ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Baraza la Taifa la Ujenzi (NCC) kwa kipindi cha pili;
 
Balozi Dkt. Jilly Elibariki Maleko ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Arusha (AICC).  Balozi Maleko anachukua nafasi ya Balozi Begum Karim Taj ambaye amemaliza muda wake;  
 
Prof. Eliakimu Mnkondo Zahabu ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Taifa cha Ufuatiliaji wa Kaboni (National Carbon Monitoring Center – NCMC); na
 
Bw. Lucas Abrahamani Mwino ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Mamlaka ya Masoko ya Mitaji na Dhamana (CMSA).  Bw. Mwino anachukua nafasi ya Dkt. John Kedi Mduma ambaye amemaliza muda wake.
Balozi Dkt. Jilly Elibariki Malek
Posted by MROKI On Tuesday, April 29, 2025 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo