Nafasi Ya Matangazo

May 27, 2024

Shirika la umeme TANESCO Wilaya ya Kigamboni imeanzisha kampeni ya mtaa kwa mtaa inayotambulika kama "Huduma  Mtaani kwako "ikiwa na lengo la kutoa elimu kwa watumiaji wahuduma za umeme, upatikanaji wa umeme na huduma zote zinaotolewa na shirika hilo.

Akizungumza mara baada ya kuwasili  eneo la mwasonga center lililopo kata ya Kisarawe II, Afisa uhusiano wilaya ya kigamboni Bi. Tumaini  Mahwaya alitambulisha huduma hiyo kwa kuelezea  umuhimu wa kutumia huduma mbali mbali za kimtandao  zinazotolewa na shirika la Umeme huku akiainisha uokoaji wa mda na fedha zinazoweza kutumika kutoka sehemu ulipo kwenda kwenye ofisi za Wilaya.






we

Aidha bi Tumaini ametoa elimu kwa wananchi namna wanavyoweza kutumia namba ya huduma kwa wateja kwa lengo la kutoa taarifa ya changamoto wanazokabiliana nazo ikiwemo itilafu ya umeme katika maeneo yao.

Naye Afisa wa huduma kwa wateja Ndg. Godwin Marandu  ametoa rai kwa wananchi kutoa taarifa za uhalifu kwa vyombo vya ulinzi hasa kwa wale wasio na nia njema kwa shirika na  wanaojihusisha na uharibifu wa miundo mbinu ya usambazaji wa nishati ya umeme sambamba na wezi wa vifaa.

Kwa Wilaya ya Kigamboni  kwa upande wa utekelezaji wa miradi ya kimkakati, utekelezaji unafanyika  kwa awamu kulingana na mahitaji ya wananchi na kwa maendeleo ya wilaya.

Kwa upande wa Kata ya Mwasonga Answary Abdallah ambaye ni Msimamizi wa utekelezaji wa miradi   Kigamboni amesema.

"TANESCO inatekeleza miradi hiyo kwa kutumia vifaa bora na vya kisasa ikiwemo utumiaji wa nguzo za zege ili kuepuka uharibifu wa miundo mbinu ya mara kwa mara kutokana na maji na uchomaji wa moto kwa nguzo za mbao".

Aidha ofisi ya TANESCO wilaya ya kigamboni inawaomba wananchi wa Mwasonga kutoa ushirikiano katika utekelezaji wa miradi ili kuleta ufanisi....
Posted by MROKI On Monday, May 27, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo