Nafasi Ya Matangazo

April 15, 2024









Mbunge wa Kigamboni Dkt Faustine Ndugulile Mb amekipongeza Chama cha Mpira wa miguu Kigamboni (KDFA) kwa kuandaa mashindano mazuri ya veterans,
 "Kwanza, nianze kuwapongeza KDFA kwa kuanzisha mashindano haya ya veteran cup ambayo leo 14, Aprili 2024 yamefika tamati. Mashindano yaliyojumuisha timu kumi na moja (11) kutoka wilaya yetu ya kigamboni kiukweli yalikuwa mazuri sana na fainali ya leo kiukweli imetupatia burudani nzuri."
"Ndugu
zangu niwaombe tuendelee kufanya mazoezi kwa ajili ya kufahamiana, kujenga urafiki na kuimarisha afya zetu".
Mashindano haya yamekutanisha baadhi ya wachezaji wa zamani wa timu za Simba na Yanga.

Fainali ilikutanisha Gezaulole veterans na kibada veterans, ambapo mchezo ulimalizika dakika tisini 90 bila kufungana na Gezaulole veterans kuibuka bigwa wa mashindano kwa kushinda mikwaju ya penati 5 na nne kwa  Kibada veterans.

Aidha, Dkt Ndugulile amemwagiza mwakilishi wa  Afisa utamaduni, Sanaa na michezo wa wilaya ya Kigamboni Bi Twidike Ntwima kuhakikisha viwanja vyote vya michezo vifuatiliwe na vitambuliwe ili vikabidhiwe Kwa timu za maeneo husika kwa matumizi, kuvitunza na kuviendeleza ili kuepuka uvamizi wa viwanja vya michezo.
Posted by MROKI On Monday, April 15, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo