Nafasi Ya Matangazo

April 08, 2024














Diwani wa kata ya  Mjimwema Mhe.Omary Ngurangwa kwa kushirikiana na kamati maalum ya mashindano ya Quran wameandika historia ya kuanzisha mashindano hayo huku suala la malezi bora likitamalaki na kuzungumzwa kwa kila mualikwa aliyepata fursa ya kuongea na Umma.

Akizungumza mbele ya Mgeni rasmi  Mh. Ngurangwa  alisisitiza suala la malezi bora ambayo msingi wake ni mafundisho sahihi ya kidini kwa mtoto tangu akiwa na umri mdogo, huku Quran ikiwa ni nyenzo ya kuusimika msingi huo.

Aidha Mgeni rasmi sheikh wa wilaya alisisitiza umuhimu wa kuienzi, na kuikuza quran kwa vijana wadogo ni jambo jema  lenye kheri na taathira kubwa kwa jamii.

Pamoja na hayo Mh. Diwani aliwashukuru washiriki wote, walimu, wazazi na walezi lakini kipekee wadau na viongozi mbalimbali waliowezesha kufana kwa mashindano hayo.

Zawadi mbalimbali zimetoelewa kwa watoto waliofanya vizuri zikiwemo  TV, BAISKELI, MADAFTARI, MISAHAFU  na PESA TASLIMU  kwa washindi wa Juzuu 1,2,3 na 5.
Posted by MROKI On Monday, April 08, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo