Nafasi Ya Matangazo

April 16, 2024








Kamati ya Siasa ya chama cha mapinduzi Wilaya ya Kigamboni Mkoani Dar es Salaam, ikiongozwa na ,Mwenyekiti wa  Wilaya ya Kigamboni, CDE. Shabani Sikunjema leo Aprili,16,2024  imefanya ziara ya kukagua miundombinu ya barabara, shule  na baadhi ya makazi ya wananchi katika   Maeneo mbalimbali yaliyo athiriwa na mvua zinazoendelea katika Kata za Pemba Mnanzi, kibada, Kisarewe II,na Kimbiji.

Aidha kamati ya siasa imemataka Mkurugenzi wa manispaa Ndg. ERASTO Kiwale kuhakikisha maeneo ya shule yanachukuliwa tahadhali kubwa ili kulinda watoto na magonjwa ya mlipuko  yanayoweza kusababishwa na kutuama kwa maji ya mvua kwenye maeneo yanayotumiwa na wanafunzi.

Sambamba na hilo katibu wa Chama cha mapinduzi ndugu, Stanley Mkandawile amewataka Tarula na Tanroads kuongeza nguvu kwenye ujenzi wa  miradi ya barabara inayoendelea ili kutatua changamoto  za  ukosefu wa mawasiliano ya baranara Kwa wananchi.
Posted by MROKI On Tuesday, April 16, 2024 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo