Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,
Prof. Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja Mradi wa BRT, Eng. Barakaeli
Mmari (kulia), na Meneja wa Wakala wa Barabara Nchini (TANROADS) Mkoa wa Dar es
salaam Eng. Harun Senkuku alipokagua Daraja la Chang’ombe na barabara ya BRT II
toka Katikati ya Jiji – Mbagala KM 20.3 Jijini Dar es Salaam leo.
Mbunge wa Temeke Mhe. Doroth
Kilave akielezea kuridhishwa kwake kutokana na kasi ya ujenzi wa Barabara ya
BRT -II toka Katikati ya Jiji – Mbagala KM 20.3, wakati Waziri wa Ujenzi na
Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa alipokagua maendeleo ya ujenzi huo.
Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi,
Prof. Makame Mbarawa akisisitiza jambo kwa Meneja Mradi wa BRT, Eng. Barakaeli
Mmari alipokagua maendeleo ya ujenzi wa Daraja la Chang’ombe jijini Dar es
Salaam.
Muonekano wa Barabara ya Kilwa
katika Makutano ya barabara hiyo na ya Nelson Mandela Kurasini Jijini Dar es
Salaam ambayo ujenzi wake unaendelea.
WAZIRI wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ameelezea kuridhishwa kwake na Ujenzi wa Barabara ya Mabasi yaendayo haraka – (BRT) sehemu ya Katikati ya Jiji kwenda Mbagala na kumtaka mkandarasi anaejenga Barabara hiyo kuhakikisha inakamilika kama ilivyo pangwa.
Akizungumza jijini Dar es Salaam leo, Prof.
Mbarawa amesema katika kipindi cha miezi mitatu kutoka sasa anatarajia barabara
hiyo yenye urefu wa kilometa 20.3 itakuwa imefunguliwa yote kwa matumizi.
“Nia ya Serikali ni kupunguza msongamano Dar es
Salaam hivyo nakuagiza TANROADS na Mkandarasi kuhakikisha sehemu inayokamilika
magari yaruhusiwe kuitumia wakati ujenzi unaendelea ili kupunguza msongamano na
kuleta ufanisi katika huduma za usafiri na uchukuzi katikati ya jiji la Dar es
Salaam,” amesisitiza Prof. Mbarawa.
Aidha amewataka madereva wa magari katika barabara
ambazo ujenzi wake bado unaendelea kutoa ushirikiano wa kutosha kwa wakandarasi
ili kulinda usalama wa abiria, wajenzi na magari kwa ujumla.
“…Hatuitaji ajali zitokee hivyo tutii maelekezo ya
wataalam wetu yenye nia ya kupunguza msongamano na kulinda usalama wa watu na
magari,” amesema Prof. Mbarawa.
Prof. Mbarawa amesema ujenzi wa Barabara na
Magaraja jijini Dar es Salaam unafanywa kwa awamu hivyo wananchi waendelee
kuiunga mkono Serikali ili kufikia malengo tarajiwa yaliokusudiwa.
Kwa upande wake, Meneja Mradi wa BRT, Eng.
Barakaeli Mmari amesema ujenzi wa Daraja la Juu sehemu ya Chang’ombe makutano
ya barabara za Nyerere na Kawawa uko sahihi kulingana na usanifu wake, lengo ni
kutoa nafasi katikati kwa magari yaendayo haraka.
Amezungumzia umuhimu wa raia wema kupata taarifa
sahihi kwa TANROADS pale wanapoona
katika miradi hiyo kuna jambo linaloitaji ufafanuzi.
Naye Mbunge wa Temeke, Mhe. Doroth Kilave
ameishukuru Serikali na kuipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi kutokana na
kasi ya ujenzi wa miadi hiyo katika jimbo lake.
Takribani Shilingi Bilioni 262 zinatarajiwa
kutumika katika ujenzi wa Barabara ya kupunguza msongamano ya Kilwa na Daraji
la Chang’ombe katika makutano ya Barabara za Nyerere na Kawawa jijini Dar es
Salaam.
0 comments:
Post a Comment