Mfanyakazi wa Airtel Tanzania kutoka idara ya Utumishi, Rose Shitindi akichangia damu kwa furaha leo ambapo watumishi wa Kampuni ya Simu ya Airtel Tanzania Ofisi ya Makao Makuu, Morroco Dar es Salaam walijitolea kuchangia damu katika Mpango wa Taifa wa Damu Salama. Anaemhudumia ni Muuguzi, Peter Chami kutoka Huduma ya Taifa ya Damu Salama. Wafanyakazi wa Airtel wameshiriki katika mpango wa uchangiaji damu ili kuokoa maisha ya watu wanaohitaji damu.
Afisa Muuguzi, Peter Chami kutoka Huduma ya
Taifa ya Damu Salama akimhudumia Meneja Mauzo wa Airtel Tanzania, Wainduni Mushi
wakati wa uchangiaji damu leo Juni 17,2022 katika ukumbi wa Airtel Makao Makuu
Morroco jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa Airtel wameshiriki katika mpango wa uchangiaji damu
ili kuokoa maisha ya watu wanaohitaji damu.Meneja Biashara wa Airtel
Tanzania David Nsimba akihudumiwa na Afisa Muuguzi, Peter Chami kutoka Huduma
ya Taifa ya Damu Salama wakati wa uchangiaji damu leo Juni 17,2022 katika
ukumbi wa Airtel Makao Makuu Morroco jijini Dar es Salaam. Wafanyakazi wa
Airtel wameshiriki katika mpango wa
uchangiaji damu ili kuokoa maisha ya watu wanaohitaji damu.
Afisa Muuguzi, Peter Chami
kutoka Huduma ya Taifa ya Damu Salama akimsaidia mfanyakazi wa Airtel Tanzania
kutoka kitengo cha Mtandao, Gabriel Mshiu wakati akichangia damu katika Makao
Makuu ya Airtel Morocco jijini Dar es Salaam leo Juni 17,2022. Wafanyakazi wa
Airtel wameshiriki katika mpango wa
uchangiaji damu ili kuokoa maisha ya watu wanaohitaji damu.
***********
KAMPUNI ya Simu ya Airtel
Tanzania leo imeungana na Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS) kuchangia damu
ikiwa ni sehemu ya mapo wa kampuni hiyo kurudisha huduma kwa Jamii (CSR).
Akizungumza leo jijini Dar es
Salaam wakati wa zoezi hilo, Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Airtel Tanzania
Stella Kibacha, alisema kuwa kuchangia damu ni dhamira ya kampuni katika
kuhudumia na kusaidia jamii.
“Tumesukumwa kushiriki katika
mpango wa leo wa uchangiaji damu kwani ni wazi kwamba kumekuwa na hitaji la damu katika benki
ya damu salama ili kuhudumia maisha ya watu…Tunafuraha kuwa wafanyakazi wa
Airtel wameamua kuchangia damu kwa hiari na pia kuhamasisha marafiki na familia
kufanya hivyo jijini Dar es laam na maeneo mengine nchini ili kuokoa maisha ya
watu wanaohitaji damu” alisema Kibacha.
Kibacha amesema kauli mbiu ya
kimataifa ya mwaka huu ni “Kuchangia damu ni kitendo cha mshikamano”. Tanzania
kupitia Mpango wa Taifa wa Damu salama (NBTS) inahitaji damu kila siku kwa
ajili ya Huduma za matibabu na dharura za Afya.
Alisema Airtel Tanzania inajivunia
kuandaa zoezi la uchangiaji damu kwa wafanyakazi wake na kuonyesha mshikamano
katika kuadhimisha siku ya uchangiaji damu.







0 comments:
Post a Comment