Nafasi Ya Matangazo

April 15, 2019

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Dk Yussuf Singo (kulia) akimkabidhi mpira msanii, Amisa Mobeto wakati wa hafla ya kuzindua kampeni ya kuishangilia timu ya taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 17, Serengeti Boys, iliyoandaliwa na DStv kwenye hoteli ya Double Tree Masaki jijini Dar es Salaam.

Na Mwandishi Wetu
WATANZANIA wametakiwa kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu ya taifa ya vijana ya wachezaji wenye umri chini ya miaka 17 itakayoshiriki fainali za Mataifa ya Afrika ya Afcon 2019 itakayoanza jijini Dar es Salaam Jumapili.

Serengeti Boys itafungua dimba kwenye Uwanja wa Taifa kwa kucheza dhidi ya mabingwa mara mbili wa Afrika na mabingwa mara tano wa dunia Nigeria.

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Dk Singo aliyasema jijini Dar e Salaam jana wakati wa hafla ya DStv ya kuhamasisha watu kujitokeza kwa wingi kuishangilia timu hiyo iliyopo katika Kundi A pamoja na Nigeria, Angola na Uganda.
Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo nchini, Dk Yussuf Singo (wa pili kulia), Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania, Ronald Shelukindo (watatu kulia), mchezaji wazamani wa timu ya taifa ya Tanzania, Amri Kiemba (kushoto) na Salum Salum wa DStv kulia kabisa.

Hafla hiyo iliwahusisha wachezaji wazamani, wasanii na wadau wengine wa michezo kuhakikisha wanatumia nafasi au tasnia zao kuwahamasisha watu kujitokeza kwa wingi kuujaza uwanja huo wa Taifa.

Singo alisema kuwa DStv ambayo imekuwa mstari wa mbele kusaidia maendeleo ya michezo mbalimbali hapa nchini, imebuni kitu cha maana kuhakikisha watoto wetu hao wanaungwa mkono kwa watazamaji kuingia kwa wingi uwanjani na kuwashangilia.
Shumbana 
Naye Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania , Ronald Shelukindo alisema wakati akimkaribisha Singo kuwa ni jukumu la kila Mtanzania kujitokeza kuishangilia Serengeti na wale ambao hawatakuwa na nafasi ya kwenda uwanjani, basi wataziona mechi hizo kupitia DStv.

Alisema kuwa DStv imeanzisha kampeni hiyo ya uhamasishaji inayojulikana kama ‘DStv Inogile’ na imehakikisha kuwa michuano mbalimbali ya kimataifa inarushwa mubashara tena katika kifurushi cha chini kabisa cha DStv Bomba cha Sh. 19,000 tu.
Baadhi ya wachezaji wazamani walioudhuria hafla hiyo Double Tree Masaka, Dar es Salaam.

Kwa upande wa michuano ya Afcon ya U-17, Shelukindo alisema DStv itakuwa ikifanya kampeni kwa njia mbalimbali ikiwemo kwa njia ya mitandao na matangazo mbalimbali kuhamasisha na kuitia nguvu timu ya taifa ili iweze kufanya vizuri katika mashindano hayo.

Baadhi ya wachezaji wazamani waliodhuria hafla hiyo ni pamoja na Sekilojo Chambua, Edibily Lunyamila, Magoso, Kiemba, Madata Lubigisa na wengineo, wakati wasanii ni Mobeto, Nancy Sumari, John Makini na wengine.







Posted by MROKI On Monday, April 15, 2019 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo