Nafasi Ya Matangazo

May 25, 2018

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akipokea maelezo ya wizi wa pampu ya maji kutoka kwa mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe katika Kijiji cha Italagwe Kata ya Italagwe ili kuweza kuwalejeshea wanachi maji. Picha zote na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG-GAIRO.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe  amesema nashangaa kuona pamoja na changamoto mliyonayo ya maji ila kuna watu bado wanahujumu miundo mbinu yenu jambo linakosesha majibu sahihi, walioiba Pampu hiyo ya maji hawajatoka nje ya kijiji cha Italagwe... naomba OCD ufanye msako wa nyumba kwa nyumba ili kubaini mwizi na pampu ipatikane mara moja.
Kisima kilichoibiwa pampu.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe wakielekea kukagua mradi wa maji uliokuwa unasumbua.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe wakitoa pole kwa wafiwa wilayani katika kijiji cha Tabuhoteli -Gairo wakati wa ziara yake ya siku tatu anayoifanya ili kuchochea maendeleo shughuli za maendeleo wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe akiwasalimia wananchi wa Kijiji cha Tabuhoteli katika kata ya Chigela - Gairo.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akitoa salamu zake kwa wananchi.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Gairo, Rachel Nyangasi akiwasalimia wananchi wa kata yake.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe wakiongoza wananchi kuelekea katika mradi wa maji wa Ihenje.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akiwa na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe wakipokelewa kwa ngoma.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe na Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe wakimsikiliza Mhandisi wa wilaya ya Gairo, Heke Bulugu wakati akitoa maelezo ya 
Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchembe akitoa neno la shukrani.
Wananchi waliohudhuria.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Gairo, Rachel Nyangasi akiwasalimia wananchi wa kata yake.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe akizungumza na wananchi.
Na Cathbert Kajuna - Kajunason/MMG-GAIRO. Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Kebwe Stephen Kebwe ameliagiza jeshi la Polisi Wilaya ya Gairo kuwatafuta na kuwakamata watu walioharibu miundo mbinu ya maji ikiwemo kuiba pampu ya maji ya Kijiji cha Italagwe katika Wilaya ya Gairo na kuwafikisha kwenye vyombo vya kisheria. Dkt. Kebwe ametoa agizo mapema leo Mei 24 mwaka huu akiwa katika Kijiji cha Italagwe Kata ya Italagwe, wilayani humo wakati wa ziara yake ya siku tatu ya kutembelea na kuhimiza miradi ya maendeleo katika Wilaya ya Gairo Mkoani Morogoro. Amesema kuwa changamoto kubwa inayowakumba wananchi wa Wilaya ya Gairo ni pamoja na tatizo la maji, hapati majibu sahihi kuona pamoja na changamoto hiyo bado kuna watu wanaodiliki kufanya hujuma ya kuiba miundo mbinu ya maji na kuwasababishia wengine kukosa maji. "Nashangaa sana kuona pamoja na changamoto mliyonayo ya maji ila kuna watu bado wanahujumu miundo mbinu yenu jambo linakosesha majibu sahihi, walioiba Pampu hiyo ya maji hawajatoka nje ya kijiji cha Italagwe... naomba OCD ufanye msako wa nyumba kwa nyumba ili kubaini mwizi na pampu ipatikane mara moja," amesema.
“OCD Mkong’oto utembee kwenye kijiji hiki. Mkong’oto utembee pampu ipatikane. Kuna wengine watachukulia kisiasa siasa suala hili, hiyo ndiyo kazi ya Mbunge kuangalia kwamba tunachangamoto gani asaidiane na wananchi” alisema Dkt. Kebwe “wezi wapo hapa hapa kijijini. DC banana na Afisa Tarafa, Mtendaji wa Kata, Mtendaji wa Kijiji, fanyeni Mkutano wa hadhara pampu ipatikane” alisisitiza Mkuu huyo wa Mkoa. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa, mradi huo wa maji ulianza mwaka 2014 hadi 2015 ambapo uligharimiwa na Mbunge wa Jimbo la Gairo Mhe. Ahmed Shabiby na ulihudumia vitongoji viwili vya Dukani na Chang’ombe vyenye watu wasiopungua 2,500 na Oktoba mwaka 2017 mradi uposimama kutoa huduma kwa sababu ya pampu hiyo kuibiwa. Mkuu wa Wilaya ya Gairo Mhe. Siriel Mchemba amewahakikishia wananchi wa Gairo kuwa changamoto ya Maji wilayani humo inakaribia kuisha kwa kuwa takwimu pamoja na utekelezaji unaonesha upatikanaji wa maji unaongezeka. Upatikanaji wa maji mjini umeongezeka kutoka asilimia 35 hadi asilimia 40.7 na vijijini umefikia asilimia 51.4 kati ya asilimia 85 zinazohitajika hivyo mradi wa maji wa MORUWASA utakapokamilika changamoto ya maji Gairo itakuwa ni ndoto. "Nawaomba wananchi wangu wa Gairo waendelee kuwa wapole maana kila kukicha tunajaribu kutatua changamoto zinazotukuta likiwemo hili la maji ambalo halitachukua muda mrefu tutakuwa tumelimaliza kabisa," amesema.
Mhe. Mchembe ameongeza kuwa wanawake wanaweza hivyo waendeee kuwaamini hawatawaangusha wananchi, "Wilaya yetu inaongozwa asilimia 70 inaongozwa na akinamama hivyo tunajua changamoto zinazokuba ikiwemo zile za majumbani... vumilieni yatakwisha'.
Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt. Stephen Kebwe bado anaendelea na ziara yake Wilayani Gairo kwa lengo la kutembelea na kuhimiza utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo na kupokea kero za wananchi.
Posted by MROKI On Friday, May 25, 2018 No comments
Meneja Mahusiano wa Mult-Choice Tanzania, Johnson Mshana akiongea machache kuwashukuru na kuwakaribisha wadau katika hafla hiyo. 
************
Huku zikiwa zimebaki siku chache kwa kinyang’anyiro cha Kombe la Dunia 2018 kuanza nchini Urusi, Kampuni ya MultiChoice Tanzania imetangaza neema kwa Watanzania kwa kutoa ofa maalum kwa wateja wapya, huku ikitenga chaneli 6 maalum zitakazoonyesha michuano hiyo katika kiwango cha HD pamoja na kuwawezesha wateja wake wote kufuatilia michuano hiyo kwa Lugha ya Kiswahili katika vifurushi vyote vya DStv.

“Hii ni zaidi ya ofa” anasema Ronald Shelukindo, Mkuu wa Uendeshaji wa MultiChoice Tanzania wakati akitangaza ofa hiyo jijini Dar es Salaam jana. “Sasa tunataka watanzania waweze kupata burudani ya kombe la dunia 2018 kwa namna tofauti kabisa. Kwanza kwa wateja wapya wataweza kujiunga kw shilingi 79,000 tu na kupata seti ya DStv pamoja na kifurushi cha miezi miwili bure!” alisema Shelukindo na kuongeza “Kama hiyo haitoshi, wateja wote wa DStv, sasa wataweza kupokea matangazo ya moja kwa moja kwa lugha ya Kiswahili ambapo tuna timu ya watangazaji mahiri wa soka hapa nchini watakaowaletea watanzania burudani hii”

Amesema mbali na ofa hiyo na kutangazwa kwa michuano hiyo kwa lugha ya Kiswahili, pia DStv imetenga chaneli 6 mahususi kabisa kwa ajili ya michuano hiyo pamoja na kuhakikisha kuwa wateja wanaweza kutazama DStv popote walipo wakati wowote kwa kutumia vifaa kama simu, laptop na tablet. “Hivi sasa ukipakua app yetu ya DStv Now, unaweza kutumia hadi vifaa vitano tofauti ambavyo vyote huunganishwa na dikoda yako hivyo kuwawezesha wanafamilia kutazama vipindi tofauti kwa wakati mmoja” alisema Shelukindo.

Akitoa maelezo kuhusu jinsi DStv ilivyojizatiti kuwahakikishia watanzania burudani isiyo na kifani msimu huu wa kombe la dunia, Mkuu wa Masoko wa MultiChoice Tanzania Alpha Mria, amebainisha kuwa DStv itaonyesha michuano hiyo katika vifurushi vyake vyote, hivyo wateja wote wa DStv watafurahia michuano hiyo tena katika muonekano angavu yanni HD. 

“Kwakeli msimu huu wa kombe la Dunia, kila atakayekuwa na DStv atakuwa anapata hasa kile anachostahili kwani mechi zote zitaonekana live, kwenye HD na kwenye vifurushi vyote, huku pia zikitangazwa kwa lugha mbalimbali ikiwemo lugha ya Kiswahili” alisema Alpha 

Amesema kwa wale wanaotaka kufuatilia kwa Kiingereza wataweza kuona kupitia DStv, wale wa Kireno wataona kupitia DStv, wale wa Kifaransa pia wataona kupitia DStv, na kikubwa zaid sisi watanzania tutaweza kufuatilia kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili kupitia DStv. “Tumejipanga, kuwapa watanzania burudani ya aina yake msimu huu wa kombe la Dunia” Alisisitiza Alpha.

Katika uzinduzi huo, DStv iliwatambulisha rasmi watangazaji wa soka ambao watakuwa wakiwaletea watanzania matangazo hayo kwa Kiswahili ambapo majina makubwa ya watangazaji na wachambuzi wa soka yamo. Waliotambulishwa ni Aboubakary Liongo, Maulid Kitenge, Ephaim Kibonde, Edo Kumwembe, Ibrahim Masoud - Maestro na Oscar Oscar.

Wakiongea baada ya kutambulishwa, watangazaji na wachambuzi hao mahiri wa soka wamesema wamejizatiti kikamilifu kuhakikisha kuwa wanawaletea matangazo na uchambuzi wa kina ili kuhakikisha kuwa kila mpenda soka anafurahia na kuyaelewa vizuri mashindano hayo.

“Mwaka huu mtoto hatumwi sokoni.. Kwa DStv, hii ni zaidi ya kombe la Dunia kwani tutakuwa tukiwaletea uchambuzi wa kina kabla, wakati na baada ya mechi. Bila shaka itakuwa ni burudani mwanzo mwisho” alikaririwa Maulid Kitenge, mmoja kati ya watangazaji hao.

Uzinduzi huo ulihudhuria na mamia ya wadau mbalimbali wa soka nchini wakiwemo wachezaji maarufu waliochezea timu mbalimbali pamoja na timu ya Taifa pamoja ni viongozi mbalimbali na wapenzi wa soka maarufu nchini. Pia wachezaji kadhaa wa klabu za Simba na Yanga walihudhuria hafla hiyo iliyokuwa ya kufana sana.
Sehemu ya wadau na wateja wa DStv wakijinafasi katika futaru maalum iliyoandaliwa na Mult-choise Tanzania jijini Dar es Salaam jana. (Imendaliwa na Robert Okanda Blogs) 


Sehemu ya Mabalozi na wateja wa DStv wakijinafasi katika futaru maalum iliyoandaliwa na Mult-choise Tanzania jijini Dar es Salaam jana. 
Sehemu ya wadau, watangazaji na wateja wa DStv wakikiwa katika picha pamoja wakati wa hafla hiyo. 
Sehemu ya wadau, watangazaji na wateja wa DStv wakikiwa katika picha pamoja wakati wa hafla hiyo. 
Mkuu wa Masoko na wa Mult-Choice Tanzania, Alpha Mria akiongea na wadau wakati wa hafla hiyo. Pamoja naye ni watangazaji na mabalozi wa kampuni hiyo. 
(Picha zote na Robert Okanda)
Posted by MROKI On Friday, May 25, 2018 No comments

May 23, 2018

MTU mmoja aliyejulikana kwa Jina la Ahamad Salum mkazi wa Kata ya Namiyonga Wilaya ya Newala Mkoani Mtwara ameuawa na Mke wake Sofia Swaleh  Kwa Kuchomwa Kisu Kifuani kutokana na Majibizano ya Kupika Chakula Kingine. Anaandika Joseph Mpangala-Mtwara

Uchunguzi wa Jeshi la Polisi umebaini kuwa kabla ya Mauaji hayo kulitokea Ugomvi baina ya Marehem na Mkewe ambapo Marehem alipikiwa Chakula na baada ya Kula Hakushiba hivyo akashinikiza Mke wake kumuandalia Chakula kingine Ndipo Ndipo Ugomvi ukaibuka na Ndipo Mke wa Marehem Sofia Swalehe akachukua Kisu na Kumchoma eneo la Kifuani na kupelekea Ahamad Salum kufariki dunia kutokana na kupoteza Damu Nyingi.

Akiongea na Waandishi wa Habari Ofisini kwake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mtwara DCP Lucas Mkondya amesema Watu wawili wanashikiliwa na Polisi Mmoja ni Jirani Mussa Bakari ambaye aliingia ndani ya Nyumba baada ya kusikia Ugomvi ukiendelea na akashirikiana na Mke wa Marehem Sofia Swalehe kuua.

Aidha Kamanda Mkondya amewataka wananchii kutumia Viongozi wa Kiserikali na Kidini kuweza kutatua matatizo mbalimbali yanayowakabili katika Jamii.

'Nitoe rai kwa wananchii Magomvi hayana tija wajaribu kukaa na Kususuluhisha sio mnakaa na kugombana kwa kitu Kidogo mpaka mnapoteza Maisha kwa kitu Kidogo kama Chakula"
Posted by MROKI On Wednesday, May 23, 2018 No comments

May 22, 2018

  Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro Prof Lughano Kusiluka  akisisitiza jambo kwa wanafunzi chuo hicho kitivo cha Sheria alipowataka kutoa msaada wa kisheria kwa wananchi mara baada ya uzinduzi wa kituo cha Sheria chuoni hapo
  Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mohamed Utaly aliyekuwa mgeni rasmi wakati wa uzinduzi wa kituo cha Msaada wa kisheria katika Chuo Kikuu cha Mzumbe,Morogoro akikata utepe ,kushoto kwake ni Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mzumbe Prof, Lughano Kusiluka
Mkuu wa kitivo cha Sheria chuo kikuu cha mzumbe Prof, Syriacus Binamungu akimkabizi Vitabu vinavyohusu masula ya Sheria Makamu Mkuu wa chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Morogoro Prof, Lughano Kusiluka.
 Mkuu wa wilaya ya Mvomero Mkoani Morogoro Mohamed Utaly akitoa rai kwa wanafunzi kitizo cha sheria kuhakikisha wanatoa msaada wa kisheria kwa wananchi bila malipo kwa kuzingatia kuwa swala walilolianzisha sio la kibiashara kwani hali za wananchi wanaolengwa ni duni.

Posted by MROKI On Tuesday, May 22, 2018 1 comment
Posted by MROKI On Tuesday, May 22, 2018 No comments

May 21, 2018

Wabunge wa Bumge la Muungano a Tanzania Mei 19,2018 walishirki katika mafunzo maalum ya ulengaji shabaha yaliyofanyika katika eneo maalum la ulengaji shabaha lililopo katika Kikosi cha JKT Makutupora kilichopo nje kidogo ya jiji la Dodoma. TAZAMA VIDEO HIYO kisha Like na Subscribe akaunti yetu.
Posted by MROKI On Monday, May 21, 2018 No comments
Posted by MROKI On Monday, May 21, 2018 No comments
The Deputy Managing Director of BANK OF AFRICA – TANZANIA, Mr. Wasia Mushi delivers his welcoming remarks at the bank’s IFTAR Dinner at the Serena Hotel in Dar es salaam.

The Deputy Managing Director of BANK OF AFRICA – TANZANIA, Mr. Wasia Mushi in a jovial moment as he welcomes some of the esteemed clients of the bank who attended the bank’s IFTAR Dinner at the Serena Hotel on 18th May 2018.

The CEO and Managing Director of BANK OF AFRICA- TANZANIA, Mr. Ammish OWUSU-AMOAH, deliver his speech during the bank’s IFTAR Dinner at Serena Hotel. The event brought together the CEO of the GROUP BANK OF AFRICA, Mr. Amine BOUABID, senior officials from BANK OF AFRICA GROUP, representatives from BOA KENYA, BOA UGANDA, BOA RWANDA and BOA GHANA, leaders from the Muslim fraternity and clients of bank.

The Board Chairperson of BANK OF AFRICA- TANZANIA, Ambassador Mwanaidi .S. Maajar deliver his speech during the bank’s IFTAR Dinner at Serena Hotel. The event brought together the CEO of the GROUP BANK OF AFRICA, Mr. Amine BOUABID, senior officials from BANK OF AFRICA GROUP, representatives from BOA KENYA, BOA UGANDA, BOA RWANDA and BOA GHANA, leaders from the Muslim fraternity and clients of bank.

Staff of BANK OF AFRICA and clients saving themselves with different assortments of food at the at the bank’s IFTAR Dinner at Serena Hotel, Friday 18th May 2018.

Staff of BANK OF AFRICA and clients saving themselves with different assortments of food at the at the bank’s IFTAR Dinner at Serena Hotel, Friday 18th May 2018.
Posted by MROKI On Monday, May 21, 2018 No comments

May 20, 2018

KAMPUNI ya MultiChoice Africa Limited imethibitisha uteuzi wa Wakurugenzi wawili ambapo Mtanzania Maharage Chande, ambaye ni Mkurugenzi Mtendaji wa MultiChoice Tanzania anakuwa Mkurugenzi mpya wa kanda ya Afrika Mashariki na Magharibi wa kampuni hiyo.

Uteuzi huo uliotangazwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa MultiChoice Africa Brand de Villiers, unabainisha kuwa Maharage anachukua nafasi ya Stephen Isaboke, aliyekuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika Mashariki ambaye sasa anakuwa Mkuu wa masuala ya Mamlaka (Group Executive Head of Regulatory).
 
Uteuzi huu unaanza rasmi Juni 1, 2018 Afisa Mtendaji Mkuu wa MultiChoice Africa Brand de Villiers amesema kuwa uteuzi wa Maharage umezingatia upeo na uwezo wake mkubwa aliouonyesha katika kipindi alipoiongoza MultiChoice
Tanzania tangu alipojiunga na kampuni hiyo mwezi Juni mwak 2016. 

“Ninaamini kwa uwezo na uzoefu aliouonyesha Maharage katika kipindi kifupi cha kuiongoza kampuni ya MultiChoice Tanzania ni dhahiri kuwa atakuwa na mchango mkubwa katika kuimarisha safu yetu ya uongozi na kusaidia katika kuongeza mbinu na ujuzi aliokuwa nao katika kuimarisha kampuni yetu na kuhakikisha tunaendelea kutimiza matakwa ya wateja wetu kote Afrika”

Kwa upande wake Maharage amesema amepokea uteuzi huo kwa mikono miwili na kwamba bila shakahayo ni matokeo ya jitihada kubwa zilizofanywa na yeye pamoja na wafanyakazi wote wa MultiChoice Tanzania. 

“Kwa hakika kaitika kipindi kifupi tumekuwa na mafanikio makubwa sana – kuanzia katika kuongeza idadi ya wateja wetu, kuimarisha huduma zetu na pia kuongeza kuchangia katika maendeleo ya jamii na uchumi wa nchi yetu kwa ujumla. 

Haya ni mafanikio tunayojivunia sisi kama kampuni na tumeyafikia kwa jitihada, nidhamu na uchapakazi. Hivyo naamini mafanikio haya ya Tanzania tunaweza pia kuyatumia kama chachu ya kuleta mafanikio kwa Afika nzima”

Baadhi ya wafanyakazi wa MultiChoice Tanzania wameonyesha Furaha yao kubwa kwa uteuzi wa Mkurugenzi huyo na kusema kuwa katika kipindi chake ameleta mageuzi makubwa katika kampuni hiyo ambayo yameleta mafanikio makubwa kwa kamppuni, wafanyakazi na jamii kwa ujumla.

Mmoja wa wafanyakazi wa kampuni hiyo Esther Mtei amesema wamefurahi kuona mkurugenzi wao amekabidhiwa uongozi wa kanda na kwamba hii ni heshima kubwa kwa Tanzania ndani ya kampuni ya MultiChoice Africa. 

“Uteuzi wa Maharage kuwa mkurugenzi wa kanda ni uthibitisho tosha kuwa Watanzania tunaweza kushika nyadhifa kubwa kama hizi na pia tunaaminika. Tunaamini uteuzi huu utakuwa ni chachu kwa watanzania kuongeza bidii katika shughuli zao kwani fursa kubwa zipo kila mahali”

Kabla ya kujiunga na MultiChoice Tanzania mwaka 2016, Maharage alifanya kazi katika ngazi za juu za uongozi katika makampuni mbalimbali ikiwemo ya simu za mkononi ya Vodacom, Benki ya NBC na pia Ofisi ya Rais Maharage ana shahada ya teknolojia ya mawasiliano (Bachelor degree in Electronics and Communication) ya chuo kikuu cha Dar es Salaam na pia shahada ya juu ya uongozi wa biashara (Masters in Business Leadership) ya chuo kikuu cha Afrika Kusini (UNISA).
Posted by MROKI On Sunday, May 20, 2018 No comments

May 18, 2018

 Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TatuMzuka, Sebastian Maganga akizungumza mbele ya Waandishi wa Habari (hawapo pichani) mapema jana jijini Dar,wakati wa kumtambulisha mshindi Shakila Amri Nyani aliyejishindia kitita cha shilingi Milioni 140 huku 'akimbust' Mama yake kwenye sehemu ya usindi wake kwa kumpa kiasi cha shilingi milioni 30.
  Shakila Amri Nyani aliyejishindia kitita cha shilingi Milioni 140 huku akifafanua zaidi kwa Waandishi wa habari (hawapo pichani),namna alivyofanikiwa kushinda kitita hicho cha TatuMzuka,aidha kufuatia ushindi huo Shakila pia  'alimbust' Mama yake kwenye sehemu ya ushindi wake kwa kumpa kiasi cha shilingi milioni 30.
 
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TatuMzuka, Sebastian Maganga akimkabidhi mfano wa hundi mshindi Shakila Amri Nyani aliyejishindia kitita cha shilingi Milioni 140 huku 'akimbust' Mama yake kwenye sehemu ya usindi wake kwa kumpa kiasi cha shilingi milioni 30.

Mchezo wa namba unaongoza nchini Tanzania wa Tatu Mzuka leo umemtangaza na kumtambulisha mbele ya vyombo vya habari mama aliyejinyakulia kitita cha milioni 140 na wakati huo ‘kumbusti’ mama yake kwenye sehemu ya ushindi wake.

Shakila Amri Nyani, ambaye ni mkazi wa Newala, Mtwara na mama wa watoto 3 alisherehekea siku ya mama duniani kwa kumpa mama yake milioni 30 kama ishara ya kutambua mchango wake katika siku hiyo muhimu.

Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano wa TatuMzuka, Bwana Sebastian Maganga alikuwepo kuwakab
idhi hundi Bi Nyani pamoja na mama yake. “Mama zetu ni hazina na hakuna kiwango chochote cha pesa kinachoweza kutosha kulipa upendo, msaada na kazi kubwa walioifanya katika kutulea. Kwa ushindi huu Tatu Mzuka tunaamini Bi Nyani na mama yake watafurahia na kuboresha maisha yao pamoja na familia zao” alisema Maganga

Bi Nyani, mwenye miaka 38 alikuwepo kuelezea furaha yake na namna ambavyo alicheza mpaka akapata ushindi huo mnono wa milioni 140.“ Nimekuwa nikicheza Tatu Mzuka kwa muda mrefu sasa. Nina furaha kubwa sana. Sikuwahi hata kuota kama naweza kupata nafasi kama hii. Mimi ni mjasiriamali na ninapanga kutumia pesa nilizoshinda kuongeza mtaji wa biashara yangu” alisema Bi Nyani

Bi Fatuma Bakari ambaye ni mama mzazi wa Nyani aliishukuru Tatu Mzuka kwa kuja na kampeni ya ‘Wiki Maalumu ya mama’ ambayo imemfanya akabustiwa kwa pesa nyingi baada ya mtoto wake kushinda.“Mimi pia nitatumia pesa nilizobustiwa kuwabusti ndugu wengine na kufanya shughuli za maendeleo ili kuboresha hali ya maisha ya familia yangu.” Alisema Bi Fatuma

Maganga alimalizia shughuli kwa kutoa dondoo ya kampeni mpya ilioanza leo – Mzukapaswedi. “Na hapa kinachohitajika ni namba zako 3 tu!! Za Bahati, ambazo zitakufanya ufikie mafanikio yako,iwe ni kuongeza elimu,kununua gari,kujenga frame za maduka, kuwekeza kwenye kilimo, nk, fanikisha matunda ya mzuka-paswedi yako kwa ushindi wa laki 1 hadi millioni 6 kila saa.
Ushindi wa millioni 10 katika mzuka deile leo saa tatu na nusu usiku, na ushindi wa millioni 60, jumapili hii kuanzia saa 3 na nusu usiku, tuma 500 hadi 30,000 kwenda namba ya kampuni 555111, na kumbukumbu namba ni namba zako 3 za bahati zikifuatiwa na neno mzukapaswedi kutoka 3mzuka, ukishinda Tanzania inashinda...
Posted by MROKI On Friday, May 18, 2018 No comments
  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo