Nafasi Ya Matangazo

September 09, 2017

Na Rhoda Ezekiel Kigoma,
MKUU wa Wilaya ya Kakonko, mkoani Kigoma, Kanali Hosea Ndagala, amewataka Wanafunzi wa kidato cha sita wa Oparation ya  Tanzania ya Viwanda waliokuwa wa kihitimu mafunzo yao katika Kambi ya Kanembwa  KJ 824 Wilayani humo kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana wengine.

Kanali Ndagala aliwataka wahitimu hao kuwa mfano kwa Wenzao pindi watakapo kwenda vyuoni kwa kujiepusha na na vitendo vya anasa na kila aina ya maovu katika jamii, kwakutumia taaluma na mafunzo waliyoyapata kwa kujiajiri kwa maendeleo yao na taifa.

Aidha  Kanali Ndagala aliwaasa Vijana hao kuendeleza uzalendo na uwajibikaji waliofundishwa na wakufunzi wao wa Jeshi la Wananchi kuwa wazalendo kwa kufichua waovu na kukomesha vitendo vya uhalifu katika maeneo yao na kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya na zinaa ili Taifa liendelee kuwa na Vijana Wenye nguvu na watakao saidia adhima ya serikali ya Tanzania ya Viwanda kukamilika.
Vijana 954 waliohitimu mafunzo hayo kwa Mujibu wa Sheria katika kambi hiyo, ambapo aliwataka  Vijana hao kujiepusha kutumiwa na makundi yasiyofaa na kufanya uhalifu watakapo kwenda vyuoni na Wakawe mfano kwa Wenzao kwa kufanya mambo yanayopendeza ikiwa ni pamoja na kujiajili kwa kuanzisha shughuli mbalimbali kutokana na mafunzo  waliyopatiwa.

 Mkuu huyo alisema lengo la serikali kuanzisha mafunzo hayo, ni kutaka Vijana kuwa na uzalendo na kujifunza namna ya kujiajiri na kuacha kusuburi hadi serikali itoe ajira na kuwafanya kupenda kufanya kazi na  kuondoa ubaguzi wa kikanda.

"Niwapongeze kwa kucheza gwaride zuri na michezo mingi hii inaonyesha ni jinsi gani mlivyo iva katika mafunzo ya Jeshi la Kujenga  Taifa, niimani yangu mtaisifia serikali kwa kushirikiana na jeshi la akiba kwani mafunzo haya ni ya thamani sana na ni fursa ya pekee, kwani wapo wengi wangetamani kuwa kama ninyi wamekosa  na hivyo mtaitekeleza sera ya uchumi wa viwanda kwa weledi mkubwa kutokana na mafunzo haya yamewajengea hali ya kulipenda na kulitumikia taifa letu na yamewajengea umoja wa kindugu hii itasaidia kuwa na taifa la amani, umoja , mshikamano na maendeleo", alisema Kanali Ndagala.


Kanali Julius Kadawi kwa niiaba ya  Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) alisema waasisi wa jeshi hilo  waliamua kuanzisha chombo kinacho husika kutoa malezi kwa vijana wa Tanzania waweze kuendana na maadili ya makabila yetu vijana wasomi walijenga kasumba ya wao kuawa bora kuliko waliosoma majukumu na melenga kuwajenga vijana kuwa na moyo wa uzalendo, kujituma, kujiajili na kuipenda nchi yao na kujitoa kwaajili ya Nchi yao.

 Akimkaribisha mgeni rasimi Mkuu wa kikosi cha KJ824  Gerald Mollo alisema  vijana wa Mujibu wa oparatini Tanzania ya viwanda Walianza 979 wavulana wanne na msicha mmoja waliacha mafunzo kwaajili ya ugojwa Wanafunzi wengine waliacha mafunzo baada ya utoro walipokwenda kujaza gomu walitoroka vijana Waliohitimu mafunzo jana ni vijana 954 na ndio walioshiriki katika kilimo cha umwagiliaji hekari 50 kambini, maandalizi ya mashamba mapya hekari miamoja shughuli hizo walizifanya kutokana na elimu waliyopo.

Nao Wanafunzi hao waliokuwa wakihitimu mafunzo hayo waliiomba serikali kutofautisha muda wa mafunzo na kipindi cha udahiri hali inayo wapelekea muda wa mafunzo kuwa mdogo na kushindwa kupata mafunzo ipasavyo na kuwaomba  Wanafunzi wanaokimbia mafunzo hayo kuacha fikira potofu kwani mafunzo hayo yanawajenga kiakili na kimaadili na kuwafanya kuwa bora sana.
Posted by MROKI On Saturday, September 09, 2017 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo