Nafasi Ya Matangazo

July 28, 2016

Uongozi na wanachama wa Chama cha wapigapicha za Habari Tanzania (PPAT) umepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba wa Mpigapicha Mkuu wa Gazeti la Tanzania Daima, Joseph Emilio Senga kilichotokea Julai 27, huko New Dehli nchini India alikokuwa akipatiwa matibabu.

Senga alikwenda nchini India kwaajili ya matibabu ya Moyo Julai 12, mwaka huu ambapo Julai 19 alifanyiwa upasuaji wa mmoja ya mishipa moyo na kumalizika salama na Julai 27 kuruhusiwa kutoka Hospitalini lakini hali yake ilibadilika na kurwejeshwa tena Hospitalini na ilipofika saa 1:15 usiku alifariki.

Kifo cha Semnga si tu pigo kwa familia yake lakini ni pigo kubwa kwa wanahabari na wapigapicha wote nchini Tanzania hasa kutokana na uchapakazi shupavu uliosheheni weledi .

PPAT inaungana na familia yake na wote waliofikwa na msiba huu mzito  katika kipindi hiki kigumu cha maombolezo .

Aidha taarifa iliyotolewa jana na Kampuni ya Free Media, wachapishaji wa gazeti la Tanzania Daima, ilisema kuwa taarifa rasmi ya lini mwili wa marehemu utarejeshwa nchini uitatolewa kesho ikiwa ni pamoja na mipango mingine ya kuaga mwili wa marehemu na kuusafirisha hadi Kijijini kwao Mkoani Mwanza kwa mazishi.

Aidha Chama cha Demokrasia na Maendeo Chadema kimetuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha Mpigapicha huyo na kumuelezea marehemu kama Shujaa wa Demokrasia na Haki.


BWANA ALITOA NA BWANA AMETYWAA JINA LA BWANA LIHIMIDIWE. 
Marehemu Joseph Senga enzi za uhai wake. Kama taasisi na kisha mtu mmoja mmoja kuanzia kwa wanachama na viongozi wa chama kwa hatua ya sasa tumejikuta tumeishiwa maneno ya kusema kuhusu kifo cha mwandishi huyu mwandamizi, lakini katikati ya mshtuko na majonzi tuliyonayo, tunaweza kusema kuwa kifo cha Senga, hasa siku kiliyotokea, kimedhihirisha jambo moja kubwa kuwa alikuwa SHUJAA WA DEMOKRASIA NA HAKI. Kifo cha Senga kimetokea siku ambayo kulikuwa na matukio makubwa mawili kuhusu demokrasia na haki nchini. Kwanza, wakati Senga anafariki usiku wa Jumatano, Julai 27, mchana wa siku hiyo hiyo Mahakama Kuu Kanda ya Iringa, ilikuwa imetoa hukumu ya kifungo cha miaka 15 jela askari anayefahamika kwa jina la Pacificius Simon kwa hatia ya kosa la kumuua bila kukusudia aliyekuwa Mwandishi wa Habari wa Kituo cha Channel ten, mkoani Iringa. Matukio hayo matatu; kuuwawa kwa Mwangosi, hukumu ya aliyemuua na kifo cha Senga, yana uhusiano mkubwa wa karibu huku Senga akiwa katikati yake, kwamba; Picha zote ambazo hadi leo zinaweza kupatikana dunia nzima kupitia mtandao wa intaneti zikionesha mauaji ya kikatili aliyofanyiwa Mwangosi, kuanzia ile ambayo inaonesha kundi la askari polisi likiwa limemzunguka Mwangosi huku mmoja wao akiwa amemlenga kwa bunduki ya kulipulia mabomu ya machozi, hadi zile ambazo zinaonesha mwili wa mwandishi Mwangosi ukiwa umefumuliwa na kutawanywa vibaya baada ya kulipuliwa, huku nyingine ikimuonesha mmoja wa askari akiugulia maumivu ya ‘bomu’ lililomuua Mwangosi, zilipigwa na Shujaa Senga. Kwa watu waliokuwepo siku ya tukio hilo baya kuwahi kuikumba tasnia ya habari nchini, watakumbuka kuwa Senga alipiga picha zile akiwa katikati ya mirindimo na moshi wa mabomu, ngurumo za risasi za moto na kundi la askari wengi ambao walikuwa wanazidi hata idadi ya wanachama na viongozi wa CHADEMA waliokuwa wamekusanyika kwa amani kwenye ofisi yao kijijini Nyololo kabla hawajavurugwa na Jeshi la Polisi likiongozwa na RPC Michael Kamhanda. Picha zile ambazo ziliiambia dunia nzima ukweli wa tukio hilo, ziliokoa watu wengi na bila shaka zilisaidia kutotokea kwa jambo kubwa ambalo watawala walishaanza kuonesha nia ya kulitekeleza, kupitia maofisa waandamizi wa Jeshi la Polisi, makao makuu na mkoani Iringa, ambao walitaka kuonesha kuwa CHADEMA ‘walijilipua’, ambapo maana yake ni kwamba wafuasi, wanachama na viongozi wa CHADEMA walikuwa na milipuko au vitu vya namna hiyo. Pili; Senga amefariki siku ambayo Watanzania bila kujali tofauti zao, wakiongozwa na CHADEMA walitangaza Operesheni UKUTA ambayo moja ya malengo yake ni kupigania haki za makundi mbalimbali ya Watanzania, wakiwemo waandishi wa habari dhidi ya mifumo kandamizi inayolelewa na watawala kupandikiza mbegu za utawala wa kidikteta nchini. Kwa muda mrefu, kupitia chombo chake alichokuwa akikifanyia kazi hadi mauti yanamkuta, Free Media, CHADEMA kama inavyofanya kazi na waandishi wa habari wa vyombo mbalimbali, ilikuwa ikishirikiana na Senga kikazi, huku naye akifanya kazi yake kwa uwezo mkuwa, akizingatia miiko na misingi ya taaluma ya uandishi wa habari, kwa weledi mkubwa. Habari picha zake mbalimbali ambazo zimekuwa zikidhihirisha ukongwe wake katika tasnia ya habari, zikiwemo za matukio ya CHADEMA, zitakuwa historia itakayotunza jina lake miongoni mwa waandishi mahiri nchini ambazo waandishi chipukizi watajifunza. Kwa masikitiko makubwa, CHADEMA inatoa salaam za pole kwa familia ya marehemu, Mhariri Mtendaji wa Kampuni ya Free Media, wafanyakazi wenzake, tasnia ya habari nchini na Watanzania wengi walioguswa na msiba huo. Mwenyezi Mungu awatie moyo wa ujasiri kuyakabili majonzi mazito ya kifo cha mpendwa Senga. Huyo ndiyo Joseph Senga. Shujaa wa demokrasia na haki. Mwenyezi Mungu ailaze roho yake mahali pema. Imetolewa leo Alhamis, Julai 28, 2016 na; Tumaini Makene Mkuu Idara ya Habari na Mawasiliano CHADEMA Make Money Online : http://ow.ly/KNICZ

Make Money Online : http://ow.ly/KNICZ
Posted by MROKI On Thursday, July 28, 2016 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo