Nafasi Ya Matangazo

November 04, 2015


Mwanamitindo wa hapa nchini, Mustafa Assanali kulia na Katibu mtendaji wa Baraza la Sanaa Tanzania, Godfrey Mngereza wakifungua pazia kuzindua Onesho la Swahili Fashion Week leo katika mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam aambalo litakuwa na mwendelezo wa kuonesha ubunifu wa mitindo kwa siku tatu mfululizo litakalokuwa likifanyika katika hoteli ya Sea Clief jijini Dar es Salaam.
 
IKIWA tunakaribia mwisho wa mwaka 2015, onyesho rasmi la mavazi Swahili Fashion Week linakuletea pande za siku tatu za mitindo, urembo, na mitindo ya maisha katika eneo moja la tukio kukiwa na onesho lisilosahaulika na kuwa na tamaduni mbalimbali ambazo zinaendelea kuifanya Tanzania kuzidi kuangaliwa kimataifa. Hivyo kila wiki ya kwanza ya mwezi wa desemba barabara zote zinaongoza kuelekea jiji la Dar es Salaam, tangu sasa katika uzinduzi wa Swahili Fashion Week 2015, huu utakuwa mwaka wa nane wa maonesho haya.


Mwanzilishi wa onyesho hili la mavazi Swahili Fashion Week alisema Mustafa Hassanali alisema “kuna methali  inasema ” “kama unataka kwenda haraka nenda mwenyewe, kama unataka kwenda mbali nenda pamoja” mwaka huu tuna nia ya kufikia jamii kusisitiza na kukuza vipaji  katika tasnia ya mitindo na zinginezo. Tuna nia ya kukuza thamani ya bidhaa, kupigania dhana ya bidhaa zinazotangenezwa afrika na kujenga bidhaa zenye mizizi ya afrika.

Msimu wa nane wa onesho la Swahili Fashion Week utaendelea kuwa mwangaza wa maonesho ya week ya mavazi kote Afrika,ndani ya Tanzania pamoja na nchi za nje ,huku wabunifu wakipatiwa hisia kutoka kwa vyombo vya habari vya kitaaifa na kimataifa toka onesho hili lilipoanzishwa mwaka 2008.Swahili Fashion Week limekuwa jukwaa kuu la ubunifu kwa wabunifu kuanziaAfrika ya Mashariki na kati ambao wameonesha kazi zao kote ulimwenguni kwa kila hadhira.

“tunaendelea kuwaomba jamii kukuza Tasnia ya  ubunifu na kuvaa fahari ya vilivyo tengenezwa  za Afrika hasa dhana ya Kitanzania. Vipaji vya ndani vinahitaji kulelewa na kuvihusisha  bidhaa zinazotambulika ulimwenguni, kutoa ni moyo si utajiri, hivyo tunatazama mbele katika kuanza  kuwasaidia kampuni ndogo ndogo na mashirika hili kuwezesha biashara hii ya mitindo ya ubunifu.” Alisema msimamizi wa Swahili Fashion Week ,Honest Nyamai.

Onesho la Swahili Fashion Week litafanyika kuanzia tarehe 4 mpaka tarehe 6 desemba katika hotel ya Sea cliff wabunifu 24 watapata nafasi ya kuonyesha nguo zao kila jioni ya siku zote 3 za onesho kuanzia saa 2:30 usiku na kuendelea. Katika kipindi cha mchana cha siku zote tatu kutakuwa na maonesho ya bidhaa, ambapo washiriki mbalimbali wataonesha na kuuza kazi zao zilizotengenezwa na mkono, za sanaa, na vidani. Siku ya mwisho itaishia na sharehe za kutangazwa  kutoa tuzo kwa washindi wa Tasnia ya mitindo katika Nyanja 21 tofauti.

Swahili Fashion Week 2015 na Tuzo limeandaliwa na 361 degrees, kushereheswa na sea cliff hotel na kudhaminiwa na EATV, East Africa Radio, Jaguar “The Art of Performance”, CMC, Vodacom Tanzania, Tanzania Printers Ltd, A1outdoor, 2M Media, BASATA (Baraza La Sanaa La Taifa), NexiaSJ, Green Telecom, Fabcars, Asila Make up, Raha, Eventlites na Darling Tanzania
Posted by MROKI On Wednesday, November 04, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo