Nafasi Ya Matangazo

November 18, 2015


Wafanyakazi wa kampuni ya Mobisol wakikabidhi vifaa vya kuzalisha umeme wa jua kwa uongozi wa zahanati ya kijiji cha Ngasamo wilayani Simiyu katika  hafla iliyofanyika kijijini hapo kuadhimisha kufikisha wateja 30,000  wanaonufaika na umeme wa kampuni hiyo.

*******************
*Mobisol yasherehekea mafanikio hayo kwa kutoa msaada wa nishati katika zahanati ya kijiji cha Ngasamo wilayani Simiyu

Kampuni ya Mobisol  yenye makao yake makuu mjini Berlini nchini ujerumani ambayo inajihusisha na uzalishaji wa umeme wa  jua tayari imewaunganisha wateja wapatao 30,000 nchini Tanzania katika kipindi cha miaka 2 tangia ianze kutoa huduma hizi barani Afrika. 
 
Kasi hii ya ongezeko la wateja wanaotumia umeme nishati ya jua kutoka kampuni hii inadhihirisha kuwa uwekezaji wake unaendana sambamba na kuunga mkono jitihada za serikali ya Tanzania za kupunguza tatizo la upatikanaji nishati ya umeme nchini.


Katika kuadhimisha mafanikio ya kufikisha idadi ya wateja 30,000 Mobisol imetoa msaada wa kuinganisha na umeme wa nishati ya jua zahanati ya serikali ya kijiji cha Ngasamo kilichopo Simiyu ambapo anatokea mteja aliyejiunganisha na umeme wa kampuni hiyo akiwa anakamilisha idadi ya wateja 30,000  katika nchi hizi mbili  za Tanzania na Rwanda ambako  inatoa huduma zake.


Akiongea wakati wahafla ya kutoa msaada huo iliyofanyika katika zahanati  hiyo,Meneja Masoko wa Mobisol, bwana Nkora Nkoranigwa amesema kuwa kampuni hiyo imejizatiti kuondoa tatizo la giza nchini na kuaikisha iawapatia wananchi umeme wa nishati ya jua wa uhakika kwa kutumia teknolojia ya kisasa na gharama nafuu.BOFYA HAPA KWA KUSOMA ZAIDI.

“Sote tunaelewa kuwa nishati ya umeme inahitajika katika kuleta maendeleo ya haraka na kuwaongezea vipato hususani wakazi wa vijijini.Tutahakikikisa tunaunga mkono jitihada za serikali za kuzalisha na kusambaza umeme kwa kwa wananchi hususani wanaoisi maeneo ya vijijini kwa gharama nafuu ii uwasaidia katika itihada zao za kujiendelea kimaisha”.Alisema


Bwana Nkoranigwa Alisema umeme  ikipatikana utasaidia wananchi kuachana na matumizi ya vibatari na kufurahia matumizi ya vifaa vya kisasa kama jokofu,feni ,kuchaji simu na viginevyo na kuwezesha watoto kujisomea katika mazingira mazuri wawapo majumbani na mashuleni  hali ambayo itasaidia kuongeza kiwango cha ufaulu katika masomo yao.


Mganga Mkuu wa wilaya hiyo Bwana Patrick Onyango alishukuru kwa msaada huo na kusema kuwa utawaondolea kero ya kukosa nishati ya umeme waliokuwa nayo kwa muda mrefu na itarahisisha utoaji wa huduma za matibabu kwa wagonjwa na aliahidi kuwa watahakikisha wanatunza vizuri vifaa vya nishati hiyo walivyozawadiwa “Kuna msemo kuwa akufaaye kwa dhiki ndio rafiki wa kweli”.Tunaishukuru kampuni ya Mobisol kwa msaada huu wa kusaidia wananchi wengi”Alisema. 


Naye Afisa Utawala wa Wilaya hiyo Bwana Rabani Mageja kwa niaba ya serikali alishukuru  kwa zahanati hiyo kupatiwa msaada wa nishati na aliongeza kuwa serikali wilayani humo itazidi kuunga mkono wawekezaji wanaokuja na miradi ya kusaidia kuleta maendeleo katika  jamii kama ulivyo mradi wa nishati wa Mobisol.


Kwa upande wake  mteja wa  30,000 wa kampuni ya Mobisol ambaye alisababisha hafla hiyo kufanyika kijijini hapo na zahanati kupatiwa msaada Bwana Kichoro alisema kuwa amefurahi kuona kampuni imemuenzi kwa kuleta msaada wa nishati kwenye zahanati wa kuwanufaisha wananchi wote.


Akiwa ni mteja wa umeme unaozalishwa na kampuni hiyo alisema ni wa uhakika na gharama nafuu na  unafanya maisha kuwa rahisi na kisasa na kuwataka wanakijiji wajiunge kwa aili ya kuishi maisha ya kisasa na kuweza kuanzisha miradi midogo midogo ya uzalishaji kwa utumia nishati hiyo.
Posted by MROKI On Wednesday, November 18, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo