Nafasi Ya Matangazo

January 22, 2015

Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge(wa kwanza) akishuka ngazi  baada ya kukagua kivuko cha MV-Utete ambacho hakitoi huduma ya usafirishaji kutokana na kupungua kwa kina cha maji cha mto Rufiji.
*******
Naibu waziri wa ujenzi, Eng.Gerson Lwenge  ameagiza Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA), kuandaa mpango mkakati wa haraka utakaowezesha kupatikana kwa kivuko kidogo kitakachotoa huduma katika mji wa Utete wilayani Rufiji.


Hatua hiyo inafuatia mabadiliko ya tabia nchi yaliosababisha kina cha maji ya mto Rufiji kupungua na kusababisha kivuko kikubwa cha Mv. Utete kushindwa kufanya kazi kutokana na upungufu wa maji katika mto Rufiji.

Akizungumza mara baada ya kukikagua kivuko cha Mv-Utete naibu waziri Eng.Gerson Lwenge  amesisitiza hatua za haraka za kuhakikisha kivuko kidogo kinapatikana ili kutoa huduma kwa wananchi katika kipindi kifupi na kuondoa usumbufu unaowakabili wananchi kwa sasa.

“Nawapa wiki mbili kuhakikisha mnapata ufumbuzi wa kivuko kinachofaa kutumika katika mazingira ya mto Rufiji ili kukiondoa kivuko cha Mv- Utete na kukipeleka mahali pengine ambapo kitaweza kutoa huduma kikamilifu kuliko kukiacha hapa kikiwa kizima lakini hakitoi huduma”, amesisitiza naibu waziri Eng. Lwenge.
 Naibu Waziri wa Ujenzi, Gerson Lwenge (wa pili kulia) akitoa maagizo kwa Kaimu Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme(TEMESA), Manase Ole-Kujan  baada ya kukagua kivuko cha Mv-Utete wilayani Rufiji mkoani Pwani juzi.
Kivuko cha MV-Utete  ambacho kimeegeshwa na kusitisha huduma zake kutokana na kupungua kwa kina cha maji cha mto rufiji mkoani Pwani


Naibu Waziri wa Ujenzi Eng. Gerson Lwenge (wa kwanza kulia) akimpa pole Mkuu wa mkoa wa Pwani Eng. Evarist Ndikilo kufuatia mauaji ya askari polisi wawili katika kituo cha polisi cha Ikwiriri Wilayani Rufiji.
Posted by MROKI On Thursday, January 22, 2015 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo