Nafasi Ya Matangazo

August 12, 2014

Mnamo tarehe 11/08/2014 majira ya 20:00 tulipokea taarifa kutoka katika kijiji cha Bubutole Mbuyuni Kata na Tarafa ya Farkwa Wilaya ya Chemba Mkoa wa Dodoma kuwa kuna mapigano ya wanakijiji, na mtu mmoja ameuawa na wengine kujeruhiwa.

Mapigano hayo yalikuwa baina ya wanakijiji wa asili wa eneo hilo na wasukuma ambao wamechukuliwa kama wageni jambo ambalo ni kinyume na sheia za nchi.

Aliyeuawa katika mapigano hayo kwa kuchomwa mkuki kifuani upande wa kulia ni DOGANI S/O LUPONDIJE mwenye miaka 48, Msukuma na Mkazi wa Bubutole Wilayani humo.
Watuwengine saba (7) wamejeruhiwa na wanapatiwa matibabu katika Zahanati ya Kwamtoro.

Jeshi la Polisi Mkao wa Dodoma linamsaka ADAMU S/O SWALEHE Msandawe na ALLY S/O RAMADHANI ambao wote ni wakazi wa kijiji cha Bubutole na Mkoani Arusha kwani ushahidi unaonyesha ndio waliokuwa wanachochea vurugu hizo zilizopelekea mauaji.

Chanzo cha mapigano hayo ni kile kinachodaiwa kuwa kunamradi wa upimaji ardhi katika kijiji hicho unaoendelea kwaajili ya kuhamisha watu ili lijengwe bwawa. Hivyo wenyeji wanadai itakuwaje walipwe fidia wageni ambao ni wasukuma.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mikononi na watambue kila raia ana haki ya kuishi popote ilimradi havunji sheria za nchi.

Imetolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma
Posted by MROKI On Tuesday, August 12, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo