Nafasi Ya Matangazo

August 12, 2014


Meneja msaidizi wa Castle lite, Victoria Kimaro wakizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam kwenye uzinduzi wa kampeni ya kutafuta washindi wa kushiriki VIP Yachy Party ambapo kutakuwa na tamasha la burudani mbalimbali litakalofanyika katikati ya bahari ya hindi kwenye boat ya kisasa mwezi ujao. Wengine kutoka kushoto ni Meneja masoko wa bia ya Castle lite Tanzania, Vimal Vighmaria na  Meneja wa kinywaji hicho Geofray Makau.
 ******
 Na Mwandishi Wetu
KAMPUNI ya Bia Tanzania kupitia kinywaji chake cha Castle Lite, jana imezindua rasmi promosheni kubwa itakayojulikana kama ‘Lite Up The Weekend’, huku Watanzania wakipewa nafasi ya kujishindia zawadi mbalimbali.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Meneja wa Bia ya Castle Lite, Geoffrey Makau, alisema nia kubwa ni ya kufanya hivyo ni kutaka kuwaweka Watanzania pamoja.
Alisema, promosheni hiyo itaendeshwa nchi nzima, kupitia katika kifuniko cha bia ya Castle Lite, huku kukiwa na zawadi mbalimbali zitakazotolewa kila wiki, ikiwa ni fedha taslimu, vifaa vya kusikilizia muziki na nyingine nyingi.
“Ila zawadi kubwa zaidi ni ile ya washindi kupata fursa ya kufanya sherehe kubwa ndani ya boti ya kifahari, sherehe hii itajulikana kama ‘Castle Lite VIP Yacht Party’,” alisema Makau.
Meneja huyo alisema, sherehe hii itakayoanzia ndani ya boti, itaishia katika kisiwa cha Sinda kilichopo katikati ya Bahari ya Hindi jijini Dar es Salaam, ambapo muziki, vyakula na vinywaji vitakuwa vimeandaliwa kwa ajili ya washindi hao toka mikoa mbalimbali ya Tanzania.
Alisema, mteja atatakiwa kununua bia ya Castle Lite ya chupa yenye ujazo wa mililita 375 au 330 na kuangalia ndani ya kifuniko, ambapo atakuta namba za siri, kisha atatuma namba hizo kwenda 15499 au kutembelea tovuti ya www.castlelite.co.tz ili apate nafasi ya kushinda zawadi za kila wiki au zawadi kubwa ya ‘Castle Lite Yacht Party’.
Aidha kutakuwa na zawadi za kila siku kupitia vituo vya radio, ambapo wapenzi wa Castle Lite wakipiga simu watatakiwa wapokee kwa kuanza na neno ‘Lite Up The Weekend’ na wateja watakaofanya vizuri watapata zawadi mbalimbali.
Mbali na zawadi, wale washindi watapata nafasi ya kuhudhuria matamasha mbalimbali ya muziki hapa nchini.
“Ninawaomba wapenzi wa bia hii ya Castle Lite, kushiriki mara nyingi wawezavyo ili kushinda zawadi hizi za kuvutia,” alisema Makau.
Castle Lite ni kinywaji kinachozalishwa na kusambazwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL), iliyo na nguvu kubwa ya soko hapa nchini.
Posted by MROKI On Tuesday, August 12, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo