Nafasi Ya Matangazo

March 18, 2014



Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Serikali kutoka Zantel Bw. Charles Jutta (kushoto), akiwakabidhi hundi yenye thamani ya shilingi milioni 10 Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi. Sihaba Nkinga (katikati) na Katibu Mtendaji wa Chama cha Netiboli Tanzania Bi. Anna Kibira. Fedha hizo ni kwaajili ya  kusaidia Chaneta leo jijini Dar es Salaam
 ***********
Na Frank Shija - WHVUM
Serikali yapokea msaada wa shilingi milioni 10 kutoka Zantel kwa lengo la kusaidia Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta)leo jijini Dar es Salaam. Msaada huo umetolewa ili kusaidia katika mashindano ya Netiboli ya Afrika Mashariki na Kati.

Akizungumza wakati wa makabidhiano wa msaada huu Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Bi Sihaba Nkinga ameishukuru kampuni ya  Zantel kwa kuonyesha utayari wa kusaidia na kuendeleza vipaji mbambali katika Nyanja ya michezo.

“Ninaipongeza kampuni ya Zantel kwa kuonyesha utayari wake katika kusaidia kukuza vipaji vya michezo hasa katika michezo ya Netiboli, Judo na Ngumi, naamini huu ni mwanzo tu.” Alisema Bi. Sihaba Nkinga.

Aidha Katibu Mkuu huyo amewaomba viongozi wa Chaneta kutumia vizuri msaada huo katika kutekeleza malengo yaliyokusudiwa ili kujenga imani kwa wadau mbambali kuendelea kusaidia sekta ya michezo

Kwa upande wake Meneja Mwandamizi wa Uhusiano wa Serikali kutoka Zantel Bw. Charles Jutta amesema kuwa kampuni yake imeshawishika kutoa msaada huo baada ya kuridhika na utendaji na muundo wa Chama cha Netiboli Tanzania (Chaneta)

Aliongeza kuwa msaada huu ni mwanzo wa Zantel kusaidi sekta ya michezo na kwa kuanzia wamechagua kusaidia michezo ya Netiboli, Judo na Ngumi na ndiyo maana leo (jana) wanatoa msaada wa shilingi milioni 10 kwa ajili ya kusaidia mashindano ya netiboli  Afrika Mashariki na Kati.

Hata hivyo Jutta amewaomba wadau mbalimbali kujitokeza kusaidia ukuzaji vipaji katika michezo mbalimbali na kusema kuwa ikiachiwa Serikali peke yake haitaweza kufanikisha azma hii njema ya kufikia mafanikio katika michezo.

Wakati huo huo Katibu Mtendaji wa Chaneta Bi. Anna Kibira ameishukuru kampuni ya Zantel kwa msaada huo na kusema kuwa msaada huo umekuja wakati muafaka ambapo chama chake kimeaanda mashindano ya kimaataifa.

Kibira aliongeza kuwa watafanya kila liwezekanalo kuhakikisha msaada huo unazaa matunda na kuleta sifa kwa taifa kwa kufanikisha mashindano hayo kuwa bora na yenye kukidhi viwango vya kimataifa.
Mashindano ya mpira wa Netiboli ya Afrika Mashariki na Kati yatafanyika kuanzia tarehe 22 mwezi huu(machi)ambapo jumla timu 22 zinatarjiwa kushiriki, kati ya timu hizo timu 10 zinaumdwa na wanaume.
Posted by MROKI On Tuesday, March 18, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo