Nafasi Ya Matangazo

March 18, 2014



KITUO cha           Uwekezaji Tanzania (TIC) kimefanikiwa kusajili miradi 9,442 tangu kuanzishwa kwake hadi 2013.

Hayo yamesemwa na Meneja Uhusiano wa TIC, Pendo Gondwe (pichani juu) wakati wa mkutano na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam.

Gondwe alisema kuwa  Watanzania wamekuwa na muamko katika uwekezaji ambapo katika miradi yote miradi ya Watanzania ni asilimia 52  na 25 ni miradi inayomilikiwa kwa ubia kati ya wageni na watanzania.

Aliongeza kuwa asilimia 23 ni miradi iliyowekezwa na wageni kutoka mataifa mbalimbali ambapo alisema miradi ambayo inaongoza kwa  uwekezaji  ni Kilimo, Maliasili, Miundombinu, Nishati, viwanda na biashara, Usafirishaji, Elimu, Afya, Miundo mbinu na madini.

Alisema TIC inawahamasisha Watanzania kujitokeza kuwekeza katika miradi mbalimbali ili kusaidia katika kukuza uchumi wa Taifa.

Gondwe alisema TIC imekuwa na utaratibu wa kuhamasisha wananchi kushiriki katika uwekezaji katika sekta nmbalimbali ambapo kituo hicho kimekuwa kikitumia mikutano na makongamano kuhamasisha wananchi kusajili miradi yao.

Kituo cha  uwekezaji kinatoa huduma mbalimbali kwa ajili ya wawekezaji wa ndani kupitia dirisha moja yaani ONE STOP CENTRE  ikiwemo kuandikisha kampuni, kujisajili na VAT, TIN, na leseni mbalimbali.
Posted by MROKI On Tuesday, March 18, 2014 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo