Meneja wa Bia ya Serengeti Rodney Rugambo akitangaza washindi wa droo ya
sita ya promosheni ya Winda Safari ya Brazili na Serengeti
inayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya Serengeti mara baada ya kuchezesha
droo hiyo mapema leo katika ofisi za kampuni hiyo jijini Dar es Salaam.
Meneja wa Bia ya Serengeti Rodney Rugambo aeleza jambo kwa wana
habari(hawapo pichani) wakati wa droo ya sita ya promosheni ya Winda
Safari ya Brazili na Serengeti inayoendeshwa na Kampuni ya Bia ya
Serengeti huku akishuhudiwa na Afisa Mkaguzi kutoka Bodi ya Michezo ya
Kubahatisha Bakari Maggid(kushoto), Maafisa waandamizi kutoka PWC(wa
pili kulia) na push mobile(wa kwanza kulia) mapema leo katika ofisi za
Kiwanda cha Bia cha Serengeti jijini Dar es Salaam.
*********
Bia ya Serengeti leo imechezesha
droo yake ya sita ya promosheni ya winda
safari ya brazil na Serengeti. Juma lililopita tulishuhudia washindi
wakijipatia ving’amuzi pamoja na simu ya kisasa aina ya Samsung galaxy tablet.
Wakati huo huo kumekuwa na washindi wengi waliojishindia zawadi za papo hapo
kama bia za bure na fedha taslimu . katika droo ya leo wamepatikana washindi
wawili wa simu aina ya Samsung galaxy tab.
Droo hiyo ilichezeshwa mapema leo
katika kiwanda cha bia cha Serengeti ikishuhudiwa na wanahabari, maofisa kutoka
bodi ya michezo ya kubahatisha, PWC na push mobile media.
Washindi wawili waliopatikana
katika droo ya sita ya winda safari ya Brazil na Serengeti ni Ms. Aquila
Machare na Emmanuel Mcharo wote kutoka Majengo katika Manispaa ya Moshi ambao wamejishindia simu aina ya Samsung galaxy
tablet.
Baada ya kupata mshindi wa kwanza
meneja wa bia Serengeti Bw Rodney Rugambo aliongea na mshindi huyo aliyekuwa na
furaha na alisisitiza kuwa amepata furaha kubwa sana kupata zawadi hiyo. “ hii
ni mara yangu ya kwanza kupata zawadi katika michezo ya bahati, sikuwahi
kufikiri na mimi nina bahati kiasi hiki na bado sijaamini kama kweli nimeshinda
zawadi hii, nawashukuru sana kampuni ya bia ya serengeti kwa kunipatia nafasi
hii” alisema Bwana Emmanuel huku akiendelea kuwasisitiza watu kuzidi kushiriki
mara nyingi Zaidi.
Pamoja na mvua kubwa na foleni zilizokuwa zikiendelea katika maeneo ya
Mbagala wiki iliyopita bado washindi wa ving’amuzi na simu walikabidhiwa zawadi
zao katika hafla fupi ya makabidhiano. Mshindi wa simu Bw Mikidadi Omar
anayetokea maeneo hayo ya Mbagala alipokea zawadi yake ya Samsung tablet na
akatumia muda huo kuwashukuru Kampuni ya Bia ya Serengeti kwa kumpa zawadi
hiyo.
Pamoja nae kulikuwa na washindi wanne wa ving’amuzi ambao ni Bakari
Abdallah Jigo kutoka Vingunguti and Rogers Isdory Kuwoko kutoka Tabata, Alex Sylvester kutoka Zanzibar na Florence
Mustapha kutoka Yombo nao walipewa
zawadi zao katika sherehe hiyo.
Promosheni ya winda safari ya Brazil na Serengeti kwa sasa ndiyo
promosheni kubwa iliyopo sokoni kwa mwaka huu, ambapo kumekuwa na washindi
Zaidi ya 100000 waliojishindia bia za bure, washindi Zaidi ya 14,000
waliojishindia fedha taslimu kiasi cha shilingi 5000 na 10000 kupitia kampeni
hii.
Meneja wa bia ya Serengeti Bw Rodney Rugambo ameeleza kuwa promosheni
hii bado inaendelea na mtu yeyote anayetumia kinywaji cha Serengeti anaweza
kujishindia zawadi mbali mbali.
“ Tunapenda kuwakumbusha wateja wetu kwamba
zawadi bado ni nyingi na wazidi kushiriki ili kuzipata zawadi hizo na haswa ile
zawadi kubwa ya tiketi ya kwenda Brazil. Pia bado tunazo simu za kisasa pamoja
na ving’amuzi vingi, hivyo tunaomba wateja wetu muendelee kunywa bia ya
Serengeti kistaarabu huku wakishiriki promosheni yetu maana waweza kuwa mshindi
wetu katika droo ijayo.pia tunapenda kuwashukuru wateja wetu kwa kuwa
promosheni yetu bado inaenda vizuri” aliendelea Rugambo.
Tafadhali kunywa kistaarabu: kushiriki lazima uwe na umri wa
miaka 18 na kuendelea.
0 comments:
Post a Comment