Nafasi Ya Matangazo

March 19, 2013

Mwimbaji wa nyimbo za injili, Upendo Nkone akiimba moja ya nyimbo zake wakati wa kuwatambulisha wanamuziki wataoshiriki tamasha la Pasaka jijini Dar es Salaam. Katikati ni Mwenyekiti wa maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama na kulia ni mwimbaji Bonny Mwaitege. (Picha na Habari Mseto Blog)
Mwimbaji wa nyimbo za injili, Bonny Mwaitege akiimba moja ya nyimbo zake wakati wa kuwatambulisha wanamuziki wataoshiriki tamasha la Pasaka jijini Dar es Salaam jana. Katikati ni Mwenyekiti wa maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama. 
Mwenyekiti wa maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kuwatambulisha baadhi ya waimbaji watakaoshirika katika tamasha la Pasaka 2013. 

Na Mwandishi Wetu

WAIMBAJI Upendo Nkone na Boniface Mwaitege wamesema wamejipanga vilivyo kufikisha neno la  Mungu kwa kupitia karama ya uimbaji katika Tamasha la Pasaka litakalofanyika Machi 31 kwenye Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam.

Nkone kwa upande wake alisema juzi kuwa amekuwa kwenye maandalizi ya uhakika ili siku ya tamasha hilo aweze kufanya vizuri kutowaangusha wapenzi na mashabiki waliomwezesha kuteuliwa kupitia ujumbe mfupi wa maneno  waliokuwa wanatuma kumpendekeza.

“Nimepata furaha kwa waamini kutambua kazi yangu, ndio maana na najihisi nina deni, hivyo nitajitahidi siku hiyo nyimba zangu zinazofahamika na mpya uitwao ‘Nimebaki na Yesu’ ambao unachochea ibada kwa waamini,” alisema Nkone.

Nkone ametoa wito kwa wapenzi, mashabiki na wadau kwa ujumla wa muziki wa injili kujitokeza kwa wingi siku hiyo kwenye Uwanja wa Taifa ambapo mgeni rasmi atakuwa Waziri Mkuu, Mizengo Pinda.

Naye Boniface Mwaitege ameshukuru kupata nafasi ya kuimba kwenye tamasha hilo la kimataifa ambalo safari hii litafanyika pia mkoani Dodoma, Mwanza, Iringa, Mbeya na Mara, akiwasihi wapenzi na mashabiki wa muziki wa injili kujitokeza kwa wingi.

“Mwaka jana nilitamani kuimba pamoja na Rebecca Malope, bahati haikuwa yangu, nashukuru safari hii nitaimba jukwaa moja na Sipho Makhabane wa  Afrika Kusini, John Lissu, Upendo Kilahiro na Rose Muhando, Nkone na wengineo,” alisema Mwaitege.

Aidha, Mkurugenzi wa Msama Promotions inayoratibu tamasha hilo, Alex Msama alisema siku ya Tamasha, kundi laGloria Celebrations litazindua albamu yake ya ‘Kuweni Macho’ ambayo pia itauzwa Uwanjani hapo.
Kuhusu viingilio, viti vya VIP, itakuwa sh 50,000, Viti maalum sh  10,000, Viti vya kawaida sh 5,000 na watoto shilingi 2000.
Posted by MROKI On Tuesday, March 19, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo