Nafasi Ya Matangazo

January 26, 2013

Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro  akiwa ndani ya treni asubuhi hii akiwapungia mkono WanaCCM wa Mkoani Dodoma waliofika kuwalaki na kuwatakia safari njema Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM
Msafara wa Baadhi ya Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM, ukiongozwa na Katibu Mkuu, Abdulrahaman Kinana  kuelekea Mkoani Kigoma katika maadhimisho ya Miaka 36 ya kuzaliwa Chama cha Mapinduzi umefika salama Mkoani Dodoma na kupata Mapokezi makubwa kutoka kw2a wana CCM mkoani hapo.

Msafara huo ulio na Wajumbe hao wane wa Sekretarieti ya CCM, na wanahabari pamoja na maofisa kadhaa wa Chama hicho ulizna safgari yake jijini Dar es Salaam Januari 25, 2013 majira ya saa 8:30 jioni na kusafiri usiku mzima njiani hadi kufika Mjini Dodoma.

Wakiwa njiani Usiku huo wajumbe hao walijumuika katika chakula katika Behewa maalum linalotoa huduma hiyo ndani ya Treni hiyo.
 Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahaman Kinana akishuka katika treni Mjini Dodoma
Akisalimiana na Baadhi ya Wana CCM akiwepo Mkuu wa Mkoa wa Dodoma
 Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM),Ndg. Abdulrahman Kinana akizungumza na Wanachama wa CCM mkoani Dodoma waliokuwa wamefika Stesheni ya Dodoma asubuhi hii kuwalaki Wajumbe wa Sekretarieti ya CCM,wanaoelekea mkoani Kigoma kwa usafiri wa treni kwenye maadhimisho ya miaka 36 ya chama cha Mapinduzi CCM,Wajumbe wa Sekretarieti ya NEC wameondoka jana jijini Dar kwenda Mkoani Kigoma kuadhimisha miaka 36 ya Chama hicho.Kushoto kwake ni Katibu wa NEC,Siasa na Mahusiano ya Kimataifa,Dkt. Asha-Rose Migiro na kulia kwake ni Katibu wa NEC,Itikaji na Uenezi CCM,Nape Nnauye
 Wana CCM Mkoa wa Dodoma  katika Mapokezi
Katibu Mkuu wa CCM aliingia katika behewa la Chakula na kujumuika na Wanahabari katika Chakula cha Usiku.
 Blogger Father Kidevu akizungumza na Wajumbe hao wa Sekretarieti ya CCM
 Muda ulienda na safari iliendelea
Maofisa wakiwa ndani ya Behewa
Posted by MROKI On Saturday, January 26, 2013 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo