Nafasi Ya Matangazo

December 01, 2012



Mwanamuziki nguli wa Kimataifa kutoka nchini DRC-Congo JB Mpiana akiimba  jukwaani mbele ya mashabiki kiduchu (hawapo pichani)  usiku wa kuamkia leo kwenye viwanja vya Lidaz Club,Kinondoni jijini Dar,ambapo kiingilio kilipangwa kuwa ni sh 25,000/= kwa laki moja wale wa VIP.
*********
BENDI ya Wenge BCBG usiku wa kuamkia janao ilikonga nyoyo za mashabiki wa muziki wa dansi waliofika kwenye viwanja vya Leaders Club kushuhudia uzinduzi wa albam ya pili ya Bendi ya Mashujaa ya Risasi Kidole, huku matatizo ya kiufundi yakisababisha bendi ya Mashujaa kushindwa kuzindua albamu hiyo.



Pamoja na kuchelewa kuanza kwa shoo hiyo, kutokana na matatizo ya kukatika kwa umeme kila muda, JB Mpiana alianza kuwatanguliza wanamuziki wake wakiongozwa na mmoja wa waanzilishi wa bendi hiyo, Shai Ngenge, na kupiga sebene kabambe kabla ya kufuatiwa na wimbo wa zamani wa Kinie  Bouger,  ambao enzi zake alishirikiana na akina, Ngiana Makanda, miaka ya katikati ya 1990.



Wimbo huo uliweza kuondoa kero kwa mashabiki hao na kuwasahaulisha yale yaliyokuwa yakiwatokea wanamuziki wa Mashujaa, ambao kila walipokuwa wakipanda jukwaani na wanapofika kuanza sebene umeme unakatika, jambo lililowafanya kupanda jukwaani mara nne, lakini wakishindwa kumaliza wibo mmoja tu wa Risasi Kidole.



JB Mpiana alionekana kuwa ni mkombozi kwa mashabiki wachache waliokuwa wamebaki huku wakipiga moyo konde kuwa hawataondoka viwanjani hapo bila ya kumuona JB, katika uzinduzi huo kutokana na burudani safi.



Kitu ambacho kiliwashangaza mashabiki wengi ni kutokatika kwa mara kwa mara kwa umeme kama ilivyotokea kwa bendi ya Mashujaa ilipokuwa jukwaani.  Mpiana aliweza kufanya kweli katika shoo hiyo kwani umeme haukukatika mpaka aliposhuka jukwaani majira ya saa 10 alfajiri.



Katika shoo hiyo, Mpiana aliweza kupiga nyimbo mbali mbali za zamani ikiwa pamoja na Barakuda, Djodjo Ngonda, Walay Danico, Dizo Dizo na zile mpya katika mtindo wa non-stop.



Mashujaa ndio walikuwa wa kwanza kupanda jukwaani na mara walipoanza kucheza shoo ya ufunguzi ambao imewajumuisha wanenguaji wa kike na wa kiume na waimbaji, umeme ulikatika na kazi ya kuanza kurejesha ikaanza na kuchukua muda wa dakika zisizopungua 30.



Tatizo hilo liliendelea mara kwa mara huku bendi hiyo ilishindwa kumaliza tatizo hilo na jitihada za kutatua hazikutoa jibu la mara moja, huku Mmoja wa viongozi wa Bendi hiyo, King Dodoo, akionekana kuhaha kila kona ya uwanja huo akiwa na Babu aliyekuwa akijitahidi kusoma dua ili Jenereta hilo liweze kufanya kazi bila kusumbua.



 Mafundi walijitahidi sana na mara baada ya mashabiki kutaka JB Mpiana apande, mafundi walitatua tatizo hilo na kumwezesha mwanamuziki huyo kufanya shoo bila tatizo hadi alipomaliza ratiba yake.



Katika tukio jingine lililojitokeza viwanjani hapo ni Mkurugenzi wa bendi hiyo, Mama Sakina, aliyeanguka ghafla, ikieleza ni presha ya ghafla kutokana na kile kilchokuwa kikiendelea mahala hapo na kukimbizwa hospitali kwa matibabu.



Uongozi wa bendi ya Mashujaa ulisema kuwa watafanya uzinduzi mwingine katika tarehe ambayo itatangazwa hapo baadaye.



 Baadhi ya Wadau na mafundi wakiwa wamelizunguka Jenereta walipokuwa wakishindwa kubaini tatizo liko wapi kutokana na hitilafu zake za mara kwa mara.


 Mashabiki wakiserebuka hivyo hivyo mara JB Mpiana na kundi lake la Wenge BCBG walipopanda jukwaani.


 Baadhi ya Wanamuziki wa JB Mpiana wakitumbuiza jukwaani


 Baadhi ya wanamuziki wa bendi ya Mashujaa wakiongozwa na Chalz Baba wakitumbuiza jukwaani,kufuatia tatizo/hitilafu ya umeme bendi hiyo ilishindwa kuzinduza albamu yake ya Kidole Risasi.


 Mdau Ben Kinyaia kutoka Clouds TV akiruka Live kunasa matukio mbalimbali yaliyokuwa yakijiri uwanjani hapo.


 Wadau waliofika kwenye uzinduzi wa albamu ya pili ya Mashujaa band


  Charls Bakishuka kutoka katika trekta alilo wasili nalo viwanja vya Leaders katika uzinduzi wa album yao ya pili. 


 Pichani juu na chini ni madansa wa bendi ya Mashujaa wakitumbuiza jukwaani.


Posted by MROKI On Saturday, December 01, 2012 No comments

0 comments:

Post a Comment

  • Facebook
  • Twitter
  • Youtube

Labels

Blog Archive

Nafasi Ya Matangazo